Thursday, December 16, 2010

JK Awaapisha Makatibu Tawala




Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete jana amewaapisha Makatibu tawala wapya wa mikoa sita katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Makatibu Tawala hao wapya walioapa jana mbele ya Rais ni pamoja na Bi.Evelyne Philbert Itanisa wa mkoa wa Arusha, Benedict Ole Kuyan wa Mkoa wa Tanga,Mgeni Sufiani Baruani wa Mkoa wa Morogoro na Liana Ayoub Hassan wa Singida.Wengine ni Nassor Mohamed Mnambila wa Kagera na Kudra Juma Mwinyimvua wa Tabora.Pichani Katibu Tawala mpya wa mkoa wa Arusha Bi.Evelyne Philbert Itanisa akila kiapo mbele ya Rais Dr.Jakaya Kikwete .

Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi miongozo ya kazi Katibu Tawala Mpya wa mkoa wa Arusha Evelyne Itanisa baada ya kula kiapo katika hafla iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam jana jioni.(Picha: Freddy Maro).

No comments:

Post a Comment