Wednesday, March 9, 2011

Tamasha la Pasaka kurindima Dodoma, Shinyanga

Rose Mhando
Solomon Mukubwa
Upendo Nkone

Na Mwndishi wetu

TAMASHA kubwa la Pasaka baada ya kufanyia Dar es salaam April 24 mwaka huu, pia litafanyika katika mikoa ya Dodoma na Shinyanga.

Mwenyekiti wa kamati ya Msama Promotions waandaaji wa tamasha hilo, Alex Msama amesema kwamba mjini Dodoma litafanyika siku ya Aprili 25 ambayo ni Jumatatu ya Pasaka na Shinyanga litafanyika Aprili 26.

Jijini Dar es Salaam Tamasha hilo litafanyika sikukuu ya Pasaka Aprili 24 katika ukumbi wa Dimond Jubilee jijini Dar es salaam.

Awali tamasha hili lilipangwa pia kufanyika jijini Mwanza, lakini kutokana na sababu maalumu sasa litafanyika katika mikoa mitatu tu… yaani Dar es Salaam, Dodoma na Shinyanga.

“Tumebadilisha ratiba kidogo kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu hatutaweza kufanya tamasha hili jijini Mwanza,” alisema Msama.

Kwa mujibu wa Msama, Tamasha la Pasaka la mwaka huu lengo lake kubwa ni kwa ajili ya kukusanya fedha za kuwasaidia watoto yatima pamoja na mitaji ya wanawake wajane.

Aidha pia fedha zitakazofanyika katika tamasha hilo zitatumika kuwasaidia wahanga wa mabomu yaliyotokea katika kambi ya jeshi Gongo la Mboto jijini Dar es salaam.

Tamasha la Pasaka la mwaka huu litashirikisha nchi sita ambazo ni Kenya, Uganda, Rwanda, DR Congo, Afrika Kusini na Zambia.

Wednesday, February 16, 2011

Sitta, Mwanjelwa nao wajitosa Tamasha la Pasaka

WAZIRI wa Afrika Mashariki na Mbunge wa Urambo kupitia CCM, Samuel Sitta amempongeza Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya tamasha la Pasaka, Alex Msama kwamba fedha zake zinazopatikana zinafanyiwa kazi zilizokusudiwa.

Tamasha la Pasaka la mwaka huu litakalofanyika Aprili 24 lengo lake kubwa kwa mujibu wa Alex Msama ni kwa ajili ya kuwasomesha watoto yatima na kuwasaidia mitaji ya biashara wanawake wajane.
Sita amesema kwamba jitihada zinazofanywa na Alex Msama ni mfano wa kuigwa kwa vijana wengi hapa nchini, kwani anaisaidia jamii kwa mapenzi kutoka moyoni.
“Kwa kweli kama wangejitokeza vijana wengine kama Msama naamini kabisa jamii yetu ingekuwa inapata misaada mingi, kwani jitihada anazozifanya ni za kumpongeza.”
Alisema ameshuhudia walemavu wakinunuliwa baiskeli, watoto yatima wakisomeshwa na wajane kusaidiwa mitaji ya biashara kupitia fedha alizozipata Msama kupitia matamasha pa Pasaka yaliyopoita.
Aliongeza kusema kwamba kwa kiasi kikubwa tamasha hilo pia litasaidia kupunguza tatizo la ajira kwa vijana, kwani wengi hivi sasa wameamua kujikita katika muziki wa injili kwa ajili ya kumuimbia Mungu na kujipatia kipato.
“Unapokuwa na watu wenye uzalendo kama Msama Promotions kwa hakika kabisa vijana wengi watajitokeza na watahamasika kujiingiza katika muziki huu, kwani watakuwa na uhakika wa kujipatia kipato,” alisema Sitta.
Wakati huo huo Mbunge wa viti maalumu kupitia chama cha Mapinduzi mkoani Mbeya, Mary Mwanjela amejitokeza kumpongeza Msama kwa kuandaa Tamasha hilo.
Pia hivi karibuni aliyekuwa Waziri Bunge, Sera na Uratibu katika awamu ya kwanza ya rais Jakaya Kikwete, Phillip Marmo alilisifia tamasha la Pasaka kwa kusema kwamba malengo yake ni mazuri kwani linasaidia jamii.

Sunday, February 6, 2011

GAZETI LA DIRA LIPO MTAANI LEO KAMA KAWAIDA YAKE

Leo kama kawaida ya gazeti hili kutoa habari zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na waandishi waliobobea katika habari za kiuchunguzi limtoka na jinsi mmiliki wa dowans alivyojipanga kuliteka bunge! unajua mmiliki huyo ni nani?, ana mipango gani? na ataliteka vipi? ....Usikose nakala yako ya DIRA YA MTANZANIAb kwa Tsh. 500/= tu

Phlip Marmo alipa tano Tamasha la Pasaka


















ALIYEKUWA Waziri wa Sera, na Uratibu waBunge katika awamu ya kwanza ya rais Jakaya Kikwete, Phillip Marmo amelisifia tamasha la Pasaka kwa kusema kwamba malengo yake ni mazuri kwani linasaidia jamii.
Tamasha la Pasaka la mwaka huu litakalofanyika Aprili 24 lengo lake kubwa kwa mujibu wa Alex Msama ambaye ndiye mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ni kwa ajili ya kuwasomesha watoto yatima na kuwasaidia mitaji ya biashara wanawake wajane.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Marmo alisema kwamba amefarijika mno na muamko wa Msama Promotions waandaaji wa tamasha hilo kwa kuangalia uwezekano wa kuwasaidia watoto yatima na wanawake wajane.
“Nimefarijika mno na muamko huu, kwakweli huu ni mfano wa kuigwa kwani ni watu wachache mno wanaoweza kuandaa matamasha kama haya na fedha zinazopatikana kuwasaidia watoto yatima na wajane,” alisema Marmo.
Aidha Marmo amesema kwamba kwa kiasi kikubwa tamasha hilo pia litasaidia kupunguza tatizo la ajira kwa vijana, kwani wengi hivi sasa wameamua kujikita katika muziki wa injili kwa ajili ya kumuimbia Mungu na kujipatia kipato.
“Unapokuwa na watu wenye uzalendo kama Msama Promotions kwa hakika kabisa vijana wengi watajitokeza na watahamasika kujiingiza katika muziki huu, kwani watakuwa na uhakika wa kujipatia kipato,” alisema Marmo.
Tamasha kubwa la Pasaka linatarajiwa kufanyika Aprili 24 mwaka huu siku ya sikuu ya Pasaka katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam na baadaye kufanyika mjini Shinyanga Jumatatu ya Pasaka Aprili 25 na jijini Mwanza Aprili 26, lengo lake kubwa mwaka huu ni kwa ajili ya kuwasomesha watoto yatima na kuwasiaid mtaji wa bishara wanawake wajane.

Friday, February 4, 2011

ISOME KATIBA YA TANZANIA.

Kutoka kushoto; Jaji Mkuu,Othman Chande, Spika wa Bunge,Anna Makinda,Rais wa Jamhuri ya Muungano,Jakaya Kikwete. Wana madaraka sawa?Katiba inasemaje?

Kama kungekuwepo na software ya kutambua neno au maneno ambayo kwa muda sasa yametawala vinywa na mijadala mbalimbali inayoendelea nchini Tanzania na hata nje ya nchi miongoni mwa watanzania, bila shaka maneno yafuatayo yangeshika nafasi za juu sana; Katiba ya Tanzania, Dowans,Tanesco,Mgao,Migomo, Bodi ya Mikopo,CHADEMA,CCM…
Kwa ujumla mijadala yote ni muhimu.Kadri tunavyojadiliana ndivyo tunavyopanua mawazo na kutafuta mbinu za kutatua masuala husika. Tatizo linakuja pale tunapojadiliana kwa jazba na kisha kuishia kulaumiana tu bila kuwa na mapendekezo halisi au huku wengine wakiona mijadala hiyo kama vitisho na hivyo kuamua kunyamazisha mijadala hiyo kwa kutumia mbinu mbalimbali.
Miongoni mwa mijadala ambayo ni muhimu sana kuwa nayo au kuiendeleza ni pamoja na huu wa Katiba ya Tanzania.Kama tunavyoelewa,Katiba ya nchi ni mama na baba wa sheria zote.Katiba ndio nchi.Muongozo. Yapo maoni mbalimbali yanayoendelea; Je kuna haja ya kuibadili katiba iliyopo,kuiandika upya au kuiwekea tu viraka hii tuliyonayo ya mwaka 1977? Tuliyonayo inasema nini,ina kasoro gani?Mijadala kama hiyo.
Wasomi mbalimbali,wataalamu wa masuala ya katiba,wameshaanza kuchangia vizuri sana kuhusu mchakato huo.Mfano mzuri ni lile Kongamano la Katiba lililoandaliwa hivi karibuni pale University of Dar-es-salaam na kushirikisha wasomi,wakufunzi na wataalamu mbalimbali wa masuala ya katiba. Kama hukuwahi kuona japo video clips mbalimbali kutoka katika kongamano lile,nakushauri U-Google “Kongamano la Katiba” ujionee na kujifunza .
Lakini tunaposubiri kutangazwa rasmi kwa tume ya katiba(nilitumaini ingeshaanza kazi) kama alivyoahidi Rais Kikwete wakati wa salamu zake za mwaka mpya, ni wazi kwamba kazi kubwa ipo mikononi mwetu;wananchi. Kama Tume itakusanya maoni,itaweka vikao mbalimbali na wananchi na kujadili au kusikiliza mapendekezo kuhusu Katiba, kuna ulazima wa wananchi hao kujua kilichomo kwenye katiba ya sasa ambayo wengi tunataka ibadilishwe kwa sababu haiendani na wakati uliopo!
Hapo ndipo umuhimu wa kuisoma Katiba unapokuja.Kwa bahati mbaya,Katiba haifundishwi mashuleni. Wanaopata nafasi ya kujifunza katiba wakiwa darasani ni wale wanaosomea Constitutional Law katika ngazi ya vyuo. Huku chini ambapo ndipo walipo au walipoishia watanzania wengi, katiba haipo katika mitaala(curriculum).
Sitoshangaa wala kukulaumu msomaji wa post hii ukiniambia kwamba hujawahi kusoma hata kifungu kimoja kutoka ndani ya Katiba. Hukupewa nafasi.Maktaba ya shule uliyosomea haikuwahi kuwa hata na copy moja ya Katiba.Ufanyeje?
Bahati nzuri ni kwamba hivi sasa tunaishi katika zama za sayansi na tekinolojia. Leo hii katiba inaweza kusomeka kutoka katika simu ya kiganjani(mobile phone). Inasomeka katika computer na pia kuna machapisho mengi zaidi ya katiba. Ukienda kwenye duka la vitabu hivi leo,bila shaka utapata copy.
Tunachotakiwa ni kuisoma Katiba(kama hujawahi kuisoma),kuwasomea wenzetu ambao kwa sababu moja ama nyingine hawajapata muda au nafasi ya kuisoma.Na unapoisoma usiisome kama vile unavyosoma kitabu cha hadithi.Hiki ni kitabu cha marejeo(reference book).Unaweza kurejea katika vifungu fulani fulani kila mara kadri inavyohitajika.
Ushauri wangu ni kwamba ukishasoma ufafanuzi wa mwanzo kuhusu katiba,inavyoundwa nk, unaweza kurukia katika vifungu fulani fulani ambavyo unahisi vinakugusa zaidi. Kama wewe ni mtu unayependa kushiriki mijadala mbalimbali kwa kutoa maoni yako, tafuta kifungu kwa mfano kinachoongelea haki yako ya kutoa maoni. Kama suala la madaraka ya Rais(inasemekana katiba ya sasa inampa madaraka makubwa sana) dhidi ya madaraka ya Bunge na Mahakama soma vifungu vinavyohusiana na madaraka ya mihimili hiyo mitatu. Ukifanya hivyo,siku Tume ikifika kwako utakuwa na cha kuchangia. La sivyo…

Wednesday, February 2, 2011

WAZIRI MFUTAKAMBA ALISIFIA TAMASHA LA PASAKA.

NAIBU Waziri wa Uchukuzi, Dk. Athuman Mfutakamba

Na Mwandishi Wetu
NAIBU Waziri wa Uchukuzi, Dk. Athuman Mfutakamba amelisifia tamasha la Pasaka kwa kusema kwamba ni jambo jema zaidi kuwasomesha watoto yatima na kuwasaidia mitaji ya biashara wanawake wajane.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mfutakamba alisema kwamba amefarijika mno na muamko wa Msama Promotions waandaaji wa tamasha hilo kwa kuangalia uwezekano wa kuwasaidia watoto yatima na wanawake wajane.
“Nimefarijika mno na muamko huu, kwakweli huu ni mfano wa kuigwa kwani ni watu wachache mno wanaoweza kuandaa matamasha kama haya na fedha zinazopatikana kuwasaidia watoto yatima na wajane,” alisema Mfutakamba.
Aidha Mtufakamba amesema kwamba kwa kiasi kikubwa tamasha hilo pia litasaidia kupunguza tatizo la ajira kwa vijana, kwani wengi hivi sasa wameamua kujikita katika muziki wa injili kwa ajili ya kumuimbia Mungu na kujipatia kipato.
“Unapokuwa na watu wenye uzalendo kama Msama Promotions kwa hakika kabisa vijana wengi watajitokeza na watahamasika kujiingiza katika muziki huu, kwani watakuwa na uhakika wa kujipatia kipato,” alisema Mfutakamba.
Tamasha kubwa la Pasaka linatarajiwa kufanyika Aprili 24 mwaka huu siku ya sikuu ya Pasaka katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam na baadaye kufanyika mjini Shinyanga Jumatatu ya Pasaka Aprili 25 na jijini Mwanza Aprili 26, lengo lake kubwa mwaka huu ni kwa ajili ya kuwasomesha watoto yatima na kuwasiaid mtaji wa bishara

Tuesday, February 1, 2011

Tanzania Yapewa Tuzo Kwa Kupambana Na Malaria


Tanzania yesterday received the First African Leaders Malaria Alliance award of excellence for its efforts in combating Malaria in the country.In the picture The United Nations Secretary General Ban-ki-Moon hands over the award to President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete in Addis Ababa Ethiopia while the chairman of the AU Commission Jena Ping(centre) looks on.(Photo: Freddy Maro

AY: WASANII TUGOMEE MALIO MADOGO KWENYE MAONYESHO.


Msanii wa kizazi kipya Ambwene Yessaya maarufu kwa jina la AY (Katikati) akiwasilisha mada kuhusu Harakati za kuufanya muziki wa Bongo Flava kuwa wa kimataifa mapema wiki hii kwenye Jukwaa la Sanaa BASATA.Kulia kwake ni Katibu Mtendaji wa BASATA,Ghonche Materego na Kaimu Mratibu wa Jukwaa hilo , Godfrey Lebejo
Katibu Mtendaji wa BASATA, Ghonche Materego (Aliyesimama) akisisitiza jambo kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila wiki kwenye Ukumbi wa BASATA.Katikati ni mwanamuziki wa kizazi kipya AY na Godfrey Lebejo ambaye ni Kaimu Mratibu wa Jukwaa hilo .
Rais wa Shirikisho la Sanaa za Maomyesho nchini, Agnes Lukanga akichangia hoja kwenye Jukwaa la Sanaa. Aliwataka wasanii kuwa na umoja katika suala la kupanga malipo katika maonyesho wanayoyafanya.
Msanii wa mziki wa hip hop a.k.a bongofleva GETHOKING a.k.a SAIDAWG akifuatilia mada katia jukwaasnaaa

Na Mwandishi Wetu
Msanii anayepata mafanikio ya kimataifa katika muziki wa kizazi kipya hapa nchini Ambwene Yessaya aka AY amewataka wasanii kugoma kulipwa fedha kidogo kwenye maonyesho na badala yake wawe na msimamo mmoja katika kupanga viwango vya malipo yao .
AY aliyasema hayo wakati akiwasilisha mada kuhusu Harakati za Kuufanya Muziki wa Kizazi kipya kuwa wa kimataifa kwenye Jukwaa la Sanaa linaofanyika kila wiki katika Ukumbi wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ambapo alisema kwamba, wasanii hapa nchini wamekuwa ni wepesi kulalamika wanapolipwa malipo kidogo lakini wagumu kuchukua hatua katika kukomesha hali hiyo.
“Wasanii wengi wanalalamika malipo kidogo kwenye maonyesho, naona hali hii wanaitaka wenyewe. Kama msanii umeweka viwango vyako vya malipo na vinatambulika lazima anayekuhitaji atakulipa tu kazi kubwa inayobaki ni kuweka juhudi na ubunifu katika kazi tunazozifanya na kwenye maonyesho” alisema AY.
Alizidi kueleza kwamba, wasanii kwa pamoja wanao uwezo wa kukataa malipo wanayolipwa sasa kwenye maonyesho kwani wao ndiyo wenye kazi na ndiyo wanaoamua kuzitumia. Katika hili alisisitiza kwamba, ni bora msanii akubali kulala njaa kwa siku moja ili aweze kula kwa mwaka mzima badala ya ilivyo sasa ambapo wamekuwa ni wa kulilia fedha za kukidhi matatizo yao madogomadogo tu.
“Huko Nigeria kulikuwa na mchezo kama huu wa wasanii kulipwa fedha ndogo kwenye maonyesho lakini kuna siku wasanii wote waliamua kugoma kushiriki shoo za nyumbani hadi hali itakapobadilika. Leo hii msanii wa Nigeria analipwa dola laki moja na nusu hadi laki mbili wakati hapa kwetu ni ndoto” alisisitiza AY huku akiwaomba wasanii kuwa na umoja katika hili.
Wakati akiwasilisha mada yake, AY alitaja mambo kama uthubutu, kutengeneza kazi za sanaa zenye ubora, kujiamini, ushirikiano, kusimamia asili yetu na vitu vingine kama nguzo zitakazosaidia kuuvusha muziki wa kizazi kipya kwenye ngazi za kimataifa.
Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa BASATA ambaye pia ni mwenyekiti wa Jukwaa hilo, Ghonche Materego alisema kwamba, Baraza lake litaendelea kuwakutanisha wasanii wa hapa nchini na wadau wa sanaa kutoka sehemu mbalimbali duniani kwa lengo la kubadilishana uzoefu na kuwapa fursa ya kujifunza kutoka kwao.
“Leo hapa tumeelezana masuala ya kujiamini, kuthubutu, kufanya kazi zenye ubora, haya yote ni ya msingi katika kukuza sanaa zetu. BASATA itaendelea kuwakutanisha wasanii na wadau wa sanaa kutoka sehemu mbalimbali duniani kwa lengo la kukuza sanaa zetu na kutekeleza kaulimbiu ya mwaka huu ya Sanaa ni Kazi” alimalizia Materego

Friday, January 28, 2011

Pinda Kufungua Mkutano Wa Wadau NSSF


KAIMU Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya jamii (NSSF), Ludovic Mrosso ambaye ni Mkurugenzi wa Fedha wa Shirika hilo, akizungumza na waandishi wa habari, leo mjini Dar es Salaam, kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya mkutano wa siku tatu wa wadau wa shirika hilo, utakaofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa mjini Arusha (AICC), kuanzia Februari 2, mwaka huu. Kulia ni Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (IT) wa NSSF, Said Masimango.

MAANDALIZI ya mkutano wa kwanza wa wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), yamekamilika ambapo hadi kufikia juzi wadau 400 walikuwa wamejisajili kushiriki mkutano huo.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Ludovic Mrosso ambaye ni Mkurugenzi wa Fedha wa Shirika hilo alisema, mkutabo huo wa siku tatu utafunbguliwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda Februari 2 mwaka huu.
Alisema mkutano huo ambao utafanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa mjini Arusha (AICC), unatarajiwa kuhudhuriwa na wadai 600 kutoka hapa nchini.
Mrosso alisema, mbali na wadau wa ndani pia NSSF imewaalika wadau kutoka nchi za Uganda, Rwanda, Burundi, Malaysia na Omani ambao kati yao wamo wataalamu mahiri na wenye uzoefu katika masuala mbalimbali ya Hifadhi za jamii.
Alisema Katika semina hiyo wataalam kutoka Malaysia watatoa mada kuhusu uzoefu wao katika namna ya uenezaji makazi huku wale wa Oman walitoa funzo kuhusu uwekezaji katika masuala ya nishati.
Mrosso alisema, hakuna ada ya ushiriki katika mkutano huo na wadau wanaolengwa ni waajiri, waajiriwa, wakuu wa vitengo vya Utawala na Fedha wa maofisi mbalimbali na Wataalam mbalimbali wa masuala ya hifadhi ya jamii.
Alisema katika mkutano huo aliouita wa kipekee kutakuwa na mada tatu kuu zitakazozungumziwa ambazo ni Uendeshaji na Uwekezaji katika NSSF Hifadhi ya jamii kwa sekta isiyo rasmi na Mamlaka ya usimamizi wa mashirika hifadhi ya jamii."NSSF itahakikisha washiriki wanafaidika na mkutano huo hususan kupitia elimu itakayotolewa na pia watapewa nafasi y a kujadili kwa kina dukuduku zao kuhusu masuala na changamoto mbalimbali zikiwemo shughuli za NSSF kwa jumla," alisema.

Monday, January 17, 2011

INVITATION FOR WINTER SICKLE CELL EVENT FOR ALL TANZANIAN-READING UK.



It is with great pleasure that we are inviting you to the Winter sickle cell event of TOSCA-UK on 23rd January 2011 at Hexham Community Centre ( Addr. 1a Bamburg Close, Reading, Berks. RG2 7UD) at 16.30 hrs. (4.30pm).
We will focus on the Tosca calendar events of the year 2011 and raffle draw for fundraising.
Kindly give us a confirmation of your attendance.
Looking forward to seeing you,
Sincerely
Alice & Zeph MwanyalalaJumuiya Ya Watanzania Reading-UKBlog :http://www.tareading.blogspot.com/Email:tzra2009@gmail.comTel No: +447865673756

GAZETI LA DIRA YA MTANZANIA LEO