Tuesday, November 30, 2010

GAZETI LA DIRAJUMATATU WIKI HII





TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akikutana kwa mara ya kwanza na baraza lake jipya la mawaziri ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi



RAIS Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumatatu, Novemba 29, 2010, amekutana rasmi kwa mara ya kwanza na Baraza la Mawaziri lake jipya pamoja na Naibu Mawaziri na kuwapa maelekezo ya awali ya nini anakitarajia kutoka kwa wateule wake hao.
Mawaziri wote 29 na Naibu Mawaziri wote 21 ambao Rais Kikwete aliwaapisha rasmi kushika nyadhifa zao katika sherehe iliyofanyika Jumamosi iliyopita, Novemba 27, 2010, wamehudhuria mkutano huo kwenye Chumba cha Baraza la Mawaziri, Ikulu, Dar es Salaam.


Katika mkutano huo uliochukua kiasi cha saa tatu, Rais alianza kwa kuwaeleza mawaziri kuwa katika kipindi hiki cha pili cha uongozi wake hakutakuwepo na muda wa kupoteza, na wala hatakuwa tayari kukubali maelezo ya kwa nini utekelezaji wa majukumu ya msingi umeshindikana.


Kwa mara nyingine amewapongeza Mawaziri na Naibu Mawaziri hao akisisitiza: “Mnastahili pongezi hasa ukizingatia ukweli kwamba nyinyi mmebahatika kuteuliwa kutoka kwenye orodha ndefu ya wabunge wengi wenye sifa za kushika nafasi mlizo nazo. Nimewateua kwa imani kuwa pamoja nanyi, tutatimiza matumaini ya wananchi wa Tanzania waliokichagua Chama cha Mapinduzi kiendelee kuongoza nchi yetu.”
Ameongeza: “Ni imani yangu kuwa kwa mshikamano na ushirikiano wetu kama timu moja ya ushindi, tutatekeleza majukumu yote kwa uadilifu, uaminifu na ufanisi wa hali ya juu. Ufanisi wa Waziri ama Naibu Waziri katika utekelezaji wa majukumu yake unategemea sana ufahamu na uelewa wake wa masuala muhimu yanayohusu Nchi, Serikali na Wizara anayoiongoza.”


Katika mkutano huo ambao ameuelezea kama wa Utangulizi wakati inaandaliwa Semina Elekezi, Rais Kikwete amewaelezea wateule wake maana ya Baraza la Mawaziri na majukumu yake, na kutaka kila Waziri ahakikishe anatayarisha kalenda yake ya masuala muhimu ambayo anataka yajadiliwe na Baraza la Mawaziri kwa mwaka.


Rais Kikwete pia amewaeleza wateule wake kuhusu wajibu wa Mawaziri katika Bunge akisisitiza kuwa ni wajibu wa kila waziri kuhudhuria vikao vyote vya Bunge, na kuwa ndani ya Bunge mawaziri wote wa Serikali lazima wawajibike kwa pamoja.


“Ni muhimu ieleweke kuwa kama ilivyo kwa maamuzi ya Baraza la Mawaziri, uwajibikaji wa Mawaziri Bungeni ni wa Pamoja. Kwa hiyo, Hoja ya Serikali Bungeni ni Hoja ya Mawaziri Wote na siyo Waziri anayewasilisha hoja tu,” amesema Rais Kikwete.


Rais pia amewakumbusha wateule wake kuhusu uwajibikaji wa pamoja (collective responsibility) katika kuongoza nchi, akisisitiza kuwa uwajibikaji huo unaelezwa kwa ufasaha katika Hati Maalum (Instrument) ya Majukumu ya kila Wizara.


Kuhusu uhusiano kati ya Waziri na Rais, na kati ya Waziri na Waziri Mkuu, Rais amesema kuwa pamoja na kwamba shughuli zote za utendaji Serikalini hutekelezwa kwa niaba ya Rais, lazima mawaziri wakumbuke kuwa Waziri Mkuu ndiye msimamizi wa shughuli za kila siku za Serikali.
Rais Kikwete pia ametaka kujengeka mahusiano mazuri kati ya Waziri na Naibu Waziri wake akisisitiza: “Jambo la msingi la kuzingatia ni kwamba uhusiano mzuri baina ya viongozi hawa ni nguzo muhimu katika mafanikio ya Wizara. Kwa hiyo, ili kuepuka migongano katika utekelezaji ni muhimu mipaka ya kazi za Waziri na Naibu Waziri ikaheshimika na pia ni wajibu wa Waziri kumpangia kazi Naibu Waziri katika Wizara husika.


Katika mkutano huo, Rais Kikwete pia amezungumzia uhusiano kati ya Waziri na Katibu Mkuu; uhusiano kati ya Waziri wa Nchi Asiyekuwa na Portfolio na Katibu Mkuu; uhusiano kati ya Naibu Waziri na Katibu Mkuu, na uhusiano kati ya Waziri na Waziri wa Sekta Nyingine.


Rais Kikwete pia amefafanua kuhusu uhusiano kati ya Wizara na Wadau Wengine; uhusiano baina ya Wizara, Mikoa na Halmashauri; uhusiano na Taasisi Zilizo Chini ya Wizara; uhusiano na Wasaidizi wa Mawaziri pamoja na utekelezaji wa Maagizo ya Viongozi wa Kitaifa.


Rais Kikwete pia amewaeleza Mawaziri na Naibu Mawaziri kuhusu nyaraka muhimu ambazo wanapaswa kukabidhiwa na kuzipitia watakapofika kwenye nafasi zao mpya za kazi. Nyaraka hizo ni pamoja na Taarifa ya Makabidhiano ya Ofisi, Katiba, Ilani ya Chama Tawala, Dira ya Taifa, na Mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini (MKUKUTA).


Aidha, Rais Kikwete amewaeleza wateule wake kuhusu umuhimu wao kufahamu Sera, Sheria, Kanuni, Taratibu, Mikakati, Mipangomkakati, Mpango na Bajeti ya Wizara, Mpango wa Kazi wa Wizara na Masharti ya Kazi ya Waziri.


Rais Kikwete vile vile amekumbusha Mawaziri na Naibu Mawaziri wake kuwa suala la vita dhidi ya rushwa ni suala la kikatiba na kuwataka kuhakikisha kuwa Mpango wa Pili wa Mkakati wa Kitaifa wa Kupambana na Rushwa (NACSAP-11) unatekelezwa.


Pia amewataka Mawaziri kusimamia mapato ya Serikali yasiyotokana na kodi na kudhibiti matumizi ya Serikali.


Rais Kikwete pia amewataka viongozi hao kuzingatia maadili ya uongozi ikiwa ni pamoja na kusimamia sheria za nchi, kuheshimu sheria katika shughuli na mambo yao binafsi na pia kutunza siri za Serikali kwa mujibu wa kiapo chao.
Rais Kikwete pia amesisitiza umuhimu wa Mawaziri na Naibu Mawaziri kuwasiliana na wananchi kwa maana ya kueleza mafanikio ya Serikali na mipango ya Serikali katika kushughulikia matatizo ya wananchi.
Amewataka kuvitumia kikamilifu Vitengo vya Mawasiliano ya Serikali katika wizara zao ambavyo ndivyo vyenye jukumu la kutoa taarifa kuhusu Wizara inavyotelekeza majukumu yake.


“Uzoefu unaonyesha kuwa Mawaziri wengi ni wazito kufanya mawasiliano na wananchi hata pale ambako Wizara imefanya mambo mengi mazuri. Hivyo, Mawaziri muwe mstari wa mbele kuelezea mafanikio ya utendaji wa Serikali katika Wizara zetu,” ameelekeza Rais Kikwete na kuongeza:


“Lazima ujengwe utamaduni wa kudumu wa kuwasiliana na wananchi wote ambao ndio waajiri wetu kupitia kura zao. Mawaziri wote tumieni Vitengo vyenu vya Mawasiliano na vyombo vya habari kwa ustadi ipasavyo,” amefafanua Rais Kikwete.


Imetolewa na:


Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,


Ikulu,


DAR ES SALAAM.


29 Novemba, 2010.

Wednesday, November 24, 2010

NCHI 56 DUNIANI ZATAJWA KUFANYA VEMA KATIKA KUUDHIBITI UKIMWI



NA MWANDISHI MAALUM

NEW YORK-Tanzania ni kati ya nchi 56 duniani ambazo zimefanikiwa ama kuudhibiti au kupunguza maambukizi mapya ya ugonjwa wa ukimwi kwa asilimia 25 katika kipindi cha kati ya 2001 hadi 2009.

Kati ya nchi hizo 56, 34 ni za Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Ripoti iliyotolewa jana na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na mpango wa kupambana na Ukimwi ( UNAIDS) imeeleza kuwa kutokana na udhibiti wa ugonjwa huo, dunia hivi sasa imeanza kushuhudia kupungua kwa maambukizi mapya kwa asilimia 20 katika kipindi cha miaka 10.

Aidha taarifa hiyo pia inaeleza kuwa katika miaka mitano iliyopita idadi vya vifo vitokanavyo na ugonjwa huo imeshuka kwa karibu asilimia 20 huku idadi ya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi ikitengamaa.

Kwa upande wa nchi tano ambazo kiwango cha maambukizo kilikuwa cha hali juu, nne kati ya hizo ambazo ni Ethiopia, Afrika ya Kusini, Zambia na Zimbabwe zimeweza kupunguza kwa asilimia 25 maambukizi mapya huku Nigeria ikielezwa kama iliyoweza kuimarisha kiwango cha maambukizi.

Bara la Afrika Kusini mwa Jangwa la Afrika ndilo linaloelezwa katika ripoti hiyo kuwa ndio limeathirika zaidi kwa kuwa na asilimia 69 ya maambukizi yote mapya.

Hata hivyo ripoti hiyo imeonyesha kuwa nchi saba ambazo zote ziko katika Ulaya ya Mashariki na Asia ya Kati kiwango cha maambukizi mapya kimeongezeka kwa asilimia 25

Ripoti hiyo inabainisha zaidi kwamba vijana katika nchi 15 ambazo zimeathiriwa zaidi za ugonjwa huo, kiwango cha maambukizi mapya kimepungua kwa asilimia 25 hasa kutokana na vijana hao kutumia njia salama za kujamiana.

Takwimu zinaonyesha katika ripoti hiyo ambayo ni mpya, kuwa kwa mwaka 2009 idadi ya watu waliopata maambukizi mapya ilikuwa milioni 2.6 ikiwa ni pungufu kwa asilimia 20 ilikilinganishwa na mwaka 1999 ambapo idadi ya watu walioambukizwa ilikuwa ni milioni 3.4.

Kwa mujibu wa ripiti hiyo watu waliokufa kutokana magonjwa yanayohusiana na ukimwi walikuwa 1.8 milioni kwa mwaka 2009 ikiwa ni pungufu ikilinganishwa na watu 2.1 milioni waliokufa mwaka 2004.

Ripoti hiyo inakwenda mbali zaidi kwa kuonyesha kuwa hadi mwishoni mwa mwaka 2009 watu 33.3 Milioni wanakadiriwa kuishi na virusi vya ukimwi, idadi ambayo ni juu kidogo ya watu 32.8 milioni kwa mwaka 2008.

Sababu ya kuwapo kwa idadi kubwa ya watu wanaoishi na virusi inaelezea katika ripoti hiyo kuwa inatokana na watu hao kutumia dawa za kuudhibiti ugonjwa huo (ARVs)

Mkurugezi Mtendaji wa UNAIDS Bw. Michel Sidibe akizungumza wakati wa uzinduzi wa ripoti hiyo uliofanyika Geneva Uswis anasema kuwa uwekezaji mkubwa wa raslimali na mipango madhubuti katika kupambana ugonjwa huo kumeza matunda.

Hata hivyo Bw. Sidibe anasema kumekuwa na upungufu katika ufadhili wa kimataifa katika mipango na miradi ya kupambana na ugonjwa huo, hali inayoweza kurudisha nyuma au hata kuzorotesha mafanikio hayo.

Baraza La Mawaziri 2010



UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116539

Fax: 255-22-2113425




PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI


NA.

OFISI/WIZARA

WAZIRI


NAIBU WAZIRI

1.

Ofisi ya Rais




1. WN – OR – Utawala Bora
Mathias Chikawe

2. WN – OR – Mahusiano na Uratibu
Stephen Wassira



2.

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma




Hawa Ghasia


3.

Ofisi ya Makamu wa Rais



1. Muungano
Samia Suluhu

2. Mazingira
Dr. Terezya Luoga Hovisa


4.

Ofisi ya Waziri Mkuu



1. Sera, Uratibu na Bunge
William Lukuvi

2. Uwekezaji na Uwezeshaji
Dr. Mary Nagu



5.

Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)



George Huruma Mkuchika

1.Aggrey Mwanri



2. Kassim Majaliwa


6.

Wizara ya Fedha



Mustapha Mkulo

1. Gregory Teu


2. Pereira Ame Silima

7.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi



Shamsi Vuai Nahodha

1. Balozi Khamis Suedi Kagasheki

8.

Wizara ya Katiba na Sheria



Celina Kombani





9.

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa




Bernard K. Membe

1. Mahadhi Juma Mahadhi

10.

Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa



Dr. Hussein Ali Hassan Mwinyi


11.

Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi




Dr. Mathayo David Mathayo

1. Benedict Ole Nangoro

12.

Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia



Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

1. Charles Kitwanga

13.

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi



Prof. Anna Tibaijuka

Goodluck Ole Madeye

14.

Wizara ya Maliasili na Utalii





Ezekiel Maige


15.

Wizara ya Nishati na Madini





William Mganga Ngeleja

1. Adam Kigoma Malima

16.

Wizara ya Ujenzi





Dr. John Pombe Magufuli

1. Dr. Harrison Mwakyembe




17.

Wizara ya Uchukuzi





Omari Nundu

1. Athumani Mfutakamba

18.

Wizara ya Viwanda na Biashara





Dr. Cyril Chami

Lazaro Nyalandu

19.

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi




Dr. Shukuru Kawambwa

1. Philipo Mulugo

20.

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii





Dr. Haji Hussein Mpanda

1. Dr. Lucy Nkya

21.

Wizara ya Kazi na Ajira





Gaudensia Kabaka

Makongoro Mahanga

22.

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto




Sophia Simba

Umi Ali Mwalimu

23.

Wizara ya Habari, Vijana na Michezo





Emmanuel John Nchimbi

1. Dr. Fenella Mukangara

24.

Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki



Samuel John Sitta






1. Dr. Abdallah Juma Abdallah

25.

Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika





Prof. Jumanne Maghembe

1. Christopher Chiza

26.

Wizara ya Maji





Prof. Mark James Mwandosya

Eng. Gerson Lwinge

Friday, November 12, 2010

Mama Salma Kikwete apokea zawadi kutoka Lindi



Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea zawadi ya jogoo aliyopewa na wazazi wa kijana Abbas Maluka wanaoishi katika kijiji cha Nangalu huko Lindi Vijijini. Abbas anasoma mwaka wa kwanza huko Dar es Salaam Institute of Technology (DIT). Mama Salma anamsaidia kijana huyo kumlipia ada ya chuo kutokana na wazazi wa Abbas kukosa uwezo wa kulipa. Makabidhiano hayo yalifanyika katika ofisi za WAMA tarehe 11.11.2010.


Chanzo ni http://mawasilianoikulu.blogspot.com/

INTERNATIONAL R&B LEGEND R. KELLY JOINS STAR STUDDED SUPERGROUP FROM AFRICA - ONE8

ONE 8....

MEDIA RELEASE

FOR IMMEDIATE RELEASE

ROCKSTAR 4000 / SONY MUSIC


The all-star line-up of the supergroup ONE8 is now complete.

The ONE8 artists have been amped up, living the high life in Chicago and most importantly, recording what will no doubt be one of the world’s hottest singles this holiday season. Hands Across the World is being released today to radio stations and clubs across Africa and worldwide.

The star-studded gathering of African musical giants has continued to gather mass momentum with 8 of Africa’s rockstar legends combining their star power and talent into the continent’s first supergroup. Now Rockstar4000 and Sony Music Worldwide are proud to announce the last signing to the group – international mega-star R. Kelly and the release of the group’s first single.

R. Kelly, who was recently joined in the world famous Chicago studios by the members of ONE8, has been a powerful force in R&B worldwide for the past two decades. Apart from global fame he has also received numerous awards for some of the most important recordings of our time, as well as outstanding production, for many years, making him one of the best selling urban artists of all time. Hits like ‘I Believe I Can Fly’, ‘Bump ‘n Grind’ and ‘Gotham City’ have made him a household name around the world and his production on top artists like Michael Jackson, Toni Braxton, LL Cool J and many more have kept him at the top of the charts and on radio for the duration of his music career.

R. Kelly is excited to be involved in the ONE8 project. Speaking from his studio in Chicago as they put the final touches to the single, he stated: “I love projects like this . As I hear the music of these artists and meet them in person I can feel myself connect. Somehow I can feel the excitement and adrenaline through them and then the ideas and everything around this track just comes together. This is probably one of the greatest things I have ever done, I can just feel it in me.

ONE8 already consists of the finest superstars on the African continent. Born from a simple idea and a small collaboration, the momentum of this project has turned it into a full-blown supergroup already dubbed by fans and media as ‘a music revolution’ and ‘history in the making’. ONE8 will release not only the hottest single of the year, but also a full album and DVD later this year. This long-term project was kicked into high gear when the artists flew into Chicago late last month to record ‘Hands Across the World’ with R. Kelly and his world class production team.

The group also recorded a video and documentary which will be released shortly.

The final ONE8 line up has been confirmed as follows:

R Kelly – USA

2Face – Nigeria

Alikiba – Tanzania

Amani – Kenya

Fally Ipupa – DRC

4X4 – Ghana

JK – Zambia

Movaizhalene – Gabon

Navio – Uganda

With a scorching hot track now released and an album in the pipeline, the ONE8 crew is heading for the ride of their lives! A major focus of the ONE8 group is to provide their fans with digital All Access passes to follow their diaries and journeys as larger than life rockstars around the clock, allowing fans closer and more personal experiences than ever before. Join online at www.myone8.com, on mobile at myone8.mobi, facebook.com/myone8, twitter.com/myone8 or youtube.com/one8TV and be part of history in the making as ONE8 explodes a revolution in music from Africa across the world!

Monday, November 8, 2010

THE THIRD ANNUAL SWAHILI FASHION WEEK ENDS ON HIGH A NOTE


Sothern Sun Best dress guest winner - Swahili Fashion Week 2010, Isabel Radick and her partner..




Emerging designer Competition Winner Subira Wahume and Mustafa Hassanali, orgnizer of Swahili Fashion Week..



Ally Hassan -(Daxx) the winner - Swahili Fashion Week 2010 model of the year award.



THE THIRD ANNUAL SWAHILI FASHION WEEK ENDS ON HIGH A NOTE

SUBIRA WAHURE: THE FUTURE OF TANZANIAN FASHION

ALI HASSAN CLINCHES THE BEST MODEL AWARD

The third annual Swahili Fashion Week at Karimjee Gardens came to a close on 6th of November 2010 in Dar Es Salaam, Tanzania with pomp and pageantry.

Swahili Fashion Week 2010 collectively brought together 24 designers from Swahili speaking countries to showcase their creativity in designing a variety of clothing with an assortment of materials and accessories.

In addition four awards were presented on the final night that included Best stands at Swahili fashion week which was warded to Art n Frame by Muzu Sulemanjee.

The winner of the Southern Sun Best Dressed Guest Award won a weekend at the hotel in an executive suite was Isabel Radick wearing Kikoromeo ensemble with her partner.

“In addition to showcasing established designers, this year Swahili Fashion Week aims giving recognition to models and emerging designers by acknowledging their hard work, dedication and commitment to the fashion industry.” said Mustafa Hassanali, organiser of the event.

Last year winner of the Swahili fashion week model award Victoria Martin, passed on her title to Ali Hassan.

From 31 applications, to 16 semi- finalist right through to the 8 Finalist who showcased their collection on the final day of Swahili fashion week, Grace kijo won the second runner up award whilst Zarina suleiman won the first runner up ward. The winner of the 2010 edition of Swahili fashion week emerging designer’s competition was Subira Wahure who won n Internship with Manju Msitta and deducted slot t 2011 edition of Swahili fashion week.

“I thank the almighty, my parents and the organisers of Swahili Fashion Week” stated an emotional Subira Wahure on being announced the winner.

Swahili fashion week 2010 has been sponsored by the home of Swahili Fashion Week - Southern Sun, Origin Africa, USAID Compete, EATV, East Africa Radio, Malaria Haikubaliki, BASATA (Baraza La Sanaa Taifa), Ultimate Security, Monier 2000, Colour Print Ltd, Global Outdoor Ltd, Amarula, Vayle Springs Ltd, ZG Films, Darling Hair, Danish make up designs, Nipashe, Bilicanas, Perfect Machinery Ltd, 1&1 Internet Solutions, Sengi Tours, iFashion and 361 Degrees.

NOTE TO EDITORS

Swahili Fashion week is a platform for designers – both fashion and accessory – from Swahili speaking countries to showcase their creativity, market their art and network with their clientele. This is all aimed at promoting fashion as an income generating, job creating industry while emphasizing a “Made in East Africa” concept.

Swahili Fashion Week is set to be an annual fashion extravaganza showcasing the best of creative talent in the fashion from Swahili Speaking countries. This being the regions highly acclaimed premier Fashion event founded created and conceptualised in year 2008 by Mustafa Hassanali

“Initiating a dynamic and promising platform for the fashion industry in the region, Swahili Fashion Week is geared towards being the most sought out fashion platform in Eastern Africa for the international market”, explained Mustafa Hassanali, founder and organizer of Swahili Fashion Week.

GAZETI LA DIRA YA MTANZANIA LEO JUMATATU



Gazeti lako mahiri la uchambuzi wa mambo ya siasa,michezo burudani na mengineyo linalochapishwa na Kampuni ya Msama Promotions,kesho liko mtaani kwa mara nyingine tena,kama ada yake huku likiwa limesheheni habari kibao za kijamii,siasa, uchumi na michezo . Jumatatu wiki hii linaingia mitaa kwa shilingi 400/= kwa kila kopi.

Saturday, November 6, 2010

Swahili Fashion Week 2010 at Karimjee Gardens Darisalaam



From (L-R) Towani, John Kaveke, Mustafa Hassanali, Sonu Sharma and Eddy.

Attentive Designers during the intergrating design and marketing workshop orgnized by USAID-COMPETE.
Fashion enthusiasts enjoying the show during the Swahili Fashion Week 2010.
Established designers, emerging designers and and other fashion stakeholders during the 'Let's Share' workshop, the second day of Swahili Fashion Week 2010 at Southern Sun Hotel.


Saphia Ngalapi
Media & PR Manager
Mustafa Hassanali
PO Box 10684, Dar es Salaam, Tanzania
105 Kilimani Road, Kinondoni, Dar es Salaam, Tanzania
(opp. Patricia Metzger Health & Beauty Clinic / near French Embassy)
Tel : +255 (0)22 266 8555
Mobile : +255 (0)712 099 834
Mail : media@mustafahassanali.net

MATUKIO YA KUAPISHWA KWA RAIS LEO





Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Davis Mwamunyange wakiingia Uwanja wa Uhuru kabla ya kuapishwa leo mchana.

Rais wa Afrika ya Kusini Mhe. Jacob Zuma akiwasili uwaja wa Uhuru leo kushuhudia kuapishwa kwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo.

Baadhi ya wakuu wa nchi za Afrika waliohudhuria sherehe hizo za kuapishwa leo mchana


Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameapishwa leo majira ya saa tano na nusu asubuhi baada ya kushinda matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31, 2010.

Rais Kikwete ameapa mbele ya jopo la viongozi wa serikali wakiwemo Jaji Mkuu, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Katibu Mkuu Kiongozi, Jopo la Majaji, Wakuu wa Vyombo vya ulinzi, Viongozi Watatu wa Madhehebu ya Dini, Wazee Wawili kutoka Tanzania Bara na Tanzania Visiwani na Karani wa Baraza la Mawaziri.
Baada ya kuapishwa, Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete alikaa kwenye kiti cha jadi na kukabidhiwa Mkuki na Ngao na wazee wa jadi kama ishara ya uongozi na mafanikio mema.
Naye Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mohamed Gharib Bilal aliapishwa mara baada ya Mheshimiwa Rais kumaliza kiapo chake.
Baada ya dua na sala kutoka kwa viongozi wa dini na madhehebu ya dini, Mheshimiwa Rais Kikwete anategemewa kupokea salamu ya Heshima kutoka kwa majeshi ambapo mizinga 21 itapigwa, bendera ya Rais itapandishwa, gwaride litaunda Umbo la Alpha na hatimaye Rais atakagua gwaride hilo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kuhutubia wananchi wa Tanzania kutokea hapa Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.
Sherehe hizi za kuapishwa rasmi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete zimehudhuriwa na marais watano wa nchi za Afrika akiwemo Mhe. Robert Mugabe wa Zimbabwe, Mhe. Mwai Kibaki wa Kenya, Mhe. Jacob Zuma wa Afrika ya Kusini, Mhe. Rupia Banda wa Zambia na Mhe. Joseph Kabila wa DRC.
Nao Umoja wa Afrika umewakilishwa na Mhe. Jean Ping ambaye ni Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika.

Chanzo ni
http://mawasilianoikulu.blogspot.com