Wednesday, March 9, 2011

Tamasha la Pasaka kurindima Dodoma, Shinyanga

Rose Mhando
Solomon Mukubwa
Upendo Nkone

Na Mwndishi wetu

TAMASHA kubwa la Pasaka baada ya kufanyia Dar es salaam April 24 mwaka huu, pia litafanyika katika mikoa ya Dodoma na Shinyanga.

Mwenyekiti wa kamati ya Msama Promotions waandaaji wa tamasha hilo, Alex Msama amesema kwamba mjini Dodoma litafanyika siku ya Aprili 25 ambayo ni Jumatatu ya Pasaka na Shinyanga litafanyika Aprili 26.

Jijini Dar es Salaam Tamasha hilo litafanyika sikukuu ya Pasaka Aprili 24 katika ukumbi wa Dimond Jubilee jijini Dar es salaam.

Awali tamasha hili lilipangwa pia kufanyika jijini Mwanza, lakini kutokana na sababu maalumu sasa litafanyika katika mikoa mitatu tu… yaani Dar es Salaam, Dodoma na Shinyanga.

“Tumebadilisha ratiba kidogo kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu hatutaweza kufanya tamasha hili jijini Mwanza,” alisema Msama.

Kwa mujibu wa Msama, Tamasha la Pasaka la mwaka huu lengo lake kubwa ni kwa ajili ya kukusanya fedha za kuwasaidia watoto yatima pamoja na mitaji ya wanawake wajane.

Aidha pia fedha zitakazofanyika katika tamasha hilo zitatumika kuwasaidia wahanga wa mabomu yaliyotokea katika kambi ya jeshi Gongo la Mboto jijini Dar es salaam.

Tamasha la Pasaka la mwaka huu litashirikisha nchi sita ambazo ni Kenya, Uganda, Rwanda, DR Congo, Afrika Kusini na Zambia.

Wednesday, February 16, 2011

Sitta, Mwanjelwa nao wajitosa Tamasha la Pasaka

WAZIRI wa Afrika Mashariki na Mbunge wa Urambo kupitia CCM, Samuel Sitta amempongeza Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya tamasha la Pasaka, Alex Msama kwamba fedha zake zinazopatikana zinafanyiwa kazi zilizokusudiwa.

Tamasha la Pasaka la mwaka huu litakalofanyika Aprili 24 lengo lake kubwa kwa mujibu wa Alex Msama ni kwa ajili ya kuwasomesha watoto yatima na kuwasaidia mitaji ya biashara wanawake wajane.
Sita amesema kwamba jitihada zinazofanywa na Alex Msama ni mfano wa kuigwa kwa vijana wengi hapa nchini, kwani anaisaidia jamii kwa mapenzi kutoka moyoni.
“Kwa kweli kama wangejitokeza vijana wengine kama Msama naamini kabisa jamii yetu ingekuwa inapata misaada mingi, kwani jitihada anazozifanya ni za kumpongeza.”
Alisema ameshuhudia walemavu wakinunuliwa baiskeli, watoto yatima wakisomeshwa na wajane kusaidiwa mitaji ya biashara kupitia fedha alizozipata Msama kupitia matamasha pa Pasaka yaliyopoita.
Aliongeza kusema kwamba kwa kiasi kikubwa tamasha hilo pia litasaidia kupunguza tatizo la ajira kwa vijana, kwani wengi hivi sasa wameamua kujikita katika muziki wa injili kwa ajili ya kumuimbia Mungu na kujipatia kipato.
“Unapokuwa na watu wenye uzalendo kama Msama Promotions kwa hakika kabisa vijana wengi watajitokeza na watahamasika kujiingiza katika muziki huu, kwani watakuwa na uhakika wa kujipatia kipato,” alisema Sitta.
Wakati huo huo Mbunge wa viti maalumu kupitia chama cha Mapinduzi mkoani Mbeya, Mary Mwanjela amejitokeza kumpongeza Msama kwa kuandaa Tamasha hilo.
Pia hivi karibuni aliyekuwa Waziri Bunge, Sera na Uratibu katika awamu ya kwanza ya rais Jakaya Kikwete, Phillip Marmo alilisifia tamasha la Pasaka kwa kusema kwamba malengo yake ni mazuri kwani linasaidia jamii.

Sunday, February 6, 2011

GAZETI LA DIRA LIPO MTAANI LEO KAMA KAWAIDA YAKE

Leo kama kawaida ya gazeti hili kutoa habari zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na waandishi waliobobea katika habari za kiuchunguzi limtoka na jinsi mmiliki wa dowans alivyojipanga kuliteka bunge! unajua mmiliki huyo ni nani?, ana mipango gani? na ataliteka vipi? ....Usikose nakala yako ya DIRA YA MTANZANIAb kwa Tsh. 500/= tu

Phlip Marmo alipa tano Tamasha la Pasaka


















ALIYEKUWA Waziri wa Sera, na Uratibu waBunge katika awamu ya kwanza ya rais Jakaya Kikwete, Phillip Marmo amelisifia tamasha la Pasaka kwa kusema kwamba malengo yake ni mazuri kwani linasaidia jamii.
Tamasha la Pasaka la mwaka huu litakalofanyika Aprili 24 lengo lake kubwa kwa mujibu wa Alex Msama ambaye ndiye mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ni kwa ajili ya kuwasomesha watoto yatima na kuwasaidia mitaji ya biashara wanawake wajane.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Marmo alisema kwamba amefarijika mno na muamko wa Msama Promotions waandaaji wa tamasha hilo kwa kuangalia uwezekano wa kuwasaidia watoto yatima na wanawake wajane.
“Nimefarijika mno na muamko huu, kwakweli huu ni mfano wa kuigwa kwani ni watu wachache mno wanaoweza kuandaa matamasha kama haya na fedha zinazopatikana kuwasaidia watoto yatima na wajane,” alisema Marmo.
Aidha Marmo amesema kwamba kwa kiasi kikubwa tamasha hilo pia litasaidia kupunguza tatizo la ajira kwa vijana, kwani wengi hivi sasa wameamua kujikita katika muziki wa injili kwa ajili ya kumuimbia Mungu na kujipatia kipato.
“Unapokuwa na watu wenye uzalendo kama Msama Promotions kwa hakika kabisa vijana wengi watajitokeza na watahamasika kujiingiza katika muziki huu, kwani watakuwa na uhakika wa kujipatia kipato,” alisema Marmo.
Tamasha kubwa la Pasaka linatarajiwa kufanyika Aprili 24 mwaka huu siku ya sikuu ya Pasaka katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam na baadaye kufanyika mjini Shinyanga Jumatatu ya Pasaka Aprili 25 na jijini Mwanza Aprili 26, lengo lake kubwa mwaka huu ni kwa ajili ya kuwasomesha watoto yatima na kuwasiaid mtaji wa bishara wanawake wajane.

Friday, February 4, 2011

ISOME KATIBA YA TANZANIA.

Kutoka kushoto; Jaji Mkuu,Othman Chande, Spika wa Bunge,Anna Makinda,Rais wa Jamhuri ya Muungano,Jakaya Kikwete. Wana madaraka sawa?Katiba inasemaje?

Kama kungekuwepo na software ya kutambua neno au maneno ambayo kwa muda sasa yametawala vinywa na mijadala mbalimbali inayoendelea nchini Tanzania na hata nje ya nchi miongoni mwa watanzania, bila shaka maneno yafuatayo yangeshika nafasi za juu sana; Katiba ya Tanzania, Dowans,Tanesco,Mgao,Migomo, Bodi ya Mikopo,CHADEMA,CCM…
Kwa ujumla mijadala yote ni muhimu.Kadri tunavyojadiliana ndivyo tunavyopanua mawazo na kutafuta mbinu za kutatua masuala husika. Tatizo linakuja pale tunapojadiliana kwa jazba na kisha kuishia kulaumiana tu bila kuwa na mapendekezo halisi au huku wengine wakiona mijadala hiyo kama vitisho na hivyo kuamua kunyamazisha mijadala hiyo kwa kutumia mbinu mbalimbali.
Miongoni mwa mijadala ambayo ni muhimu sana kuwa nayo au kuiendeleza ni pamoja na huu wa Katiba ya Tanzania.Kama tunavyoelewa,Katiba ya nchi ni mama na baba wa sheria zote.Katiba ndio nchi.Muongozo. Yapo maoni mbalimbali yanayoendelea; Je kuna haja ya kuibadili katiba iliyopo,kuiandika upya au kuiwekea tu viraka hii tuliyonayo ya mwaka 1977? Tuliyonayo inasema nini,ina kasoro gani?Mijadala kama hiyo.
Wasomi mbalimbali,wataalamu wa masuala ya katiba,wameshaanza kuchangia vizuri sana kuhusu mchakato huo.Mfano mzuri ni lile Kongamano la Katiba lililoandaliwa hivi karibuni pale University of Dar-es-salaam na kushirikisha wasomi,wakufunzi na wataalamu mbalimbali wa masuala ya katiba. Kama hukuwahi kuona japo video clips mbalimbali kutoka katika kongamano lile,nakushauri U-Google “Kongamano la Katiba” ujionee na kujifunza .
Lakini tunaposubiri kutangazwa rasmi kwa tume ya katiba(nilitumaini ingeshaanza kazi) kama alivyoahidi Rais Kikwete wakati wa salamu zake za mwaka mpya, ni wazi kwamba kazi kubwa ipo mikononi mwetu;wananchi. Kama Tume itakusanya maoni,itaweka vikao mbalimbali na wananchi na kujadili au kusikiliza mapendekezo kuhusu Katiba, kuna ulazima wa wananchi hao kujua kilichomo kwenye katiba ya sasa ambayo wengi tunataka ibadilishwe kwa sababu haiendani na wakati uliopo!
Hapo ndipo umuhimu wa kuisoma Katiba unapokuja.Kwa bahati mbaya,Katiba haifundishwi mashuleni. Wanaopata nafasi ya kujifunza katiba wakiwa darasani ni wale wanaosomea Constitutional Law katika ngazi ya vyuo. Huku chini ambapo ndipo walipo au walipoishia watanzania wengi, katiba haipo katika mitaala(curriculum).
Sitoshangaa wala kukulaumu msomaji wa post hii ukiniambia kwamba hujawahi kusoma hata kifungu kimoja kutoka ndani ya Katiba. Hukupewa nafasi.Maktaba ya shule uliyosomea haikuwahi kuwa hata na copy moja ya Katiba.Ufanyeje?
Bahati nzuri ni kwamba hivi sasa tunaishi katika zama za sayansi na tekinolojia. Leo hii katiba inaweza kusomeka kutoka katika simu ya kiganjani(mobile phone). Inasomeka katika computer na pia kuna machapisho mengi zaidi ya katiba. Ukienda kwenye duka la vitabu hivi leo,bila shaka utapata copy.
Tunachotakiwa ni kuisoma Katiba(kama hujawahi kuisoma),kuwasomea wenzetu ambao kwa sababu moja ama nyingine hawajapata muda au nafasi ya kuisoma.Na unapoisoma usiisome kama vile unavyosoma kitabu cha hadithi.Hiki ni kitabu cha marejeo(reference book).Unaweza kurejea katika vifungu fulani fulani kila mara kadri inavyohitajika.
Ushauri wangu ni kwamba ukishasoma ufafanuzi wa mwanzo kuhusu katiba,inavyoundwa nk, unaweza kurukia katika vifungu fulani fulani ambavyo unahisi vinakugusa zaidi. Kama wewe ni mtu unayependa kushiriki mijadala mbalimbali kwa kutoa maoni yako, tafuta kifungu kwa mfano kinachoongelea haki yako ya kutoa maoni. Kama suala la madaraka ya Rais(inasemekana katiba ya sasa inampa madaraka makubwa sana) dhidi ya madaraka ya Bunge na Mahakama soma vifungu vinavyohusiana na madaraka ya mihimili hiyo mitatu. Ukifanya hivyo,siku Tume ikifika kwako utakuwa na cha kuchangia. La sivyo…

Wednesday, February 2, 2011

WAZIRI MFUTAKAMBA ALISIFIA TAMASHA LA PASAKA.

NAIBU Waziri wa Uchukuzi, Dk. Athuman Mfutakamba

Na Mwandishi Wetu
NAIBU Waziri wa Uchukuzi, Dk. Athuman Mfutakamba amelisifia tamasha la Pasaka kwa kusema kwamba ni jambo jema zaidi kuwasomesha watoto yatima na kuwasaidia mitaji ya biashara wanawake wajane.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mfutakamba alisema kwamba amefarijika mno na muamko wa Msama Promotions waandaaji wa tamasha hilo kwa kuangalia uwezekano wa kuwasaidia watoto yatima na wanawake wajane.
“Nimefarijika mno na muamko huu, kwakweli huu ni mfano wa kuigwa kwani ni watu wachache mno wanaoweza kuandaa matamasha kama haya na fedha zinazopatikana kuwasaidia watoto yatima na wajane,” alisema Mfutakamba.
Aidha Mtufakamba amesema kwamba kwa kiasi kikubwa tamasha hilo pia litasaidia kupunguza tatizo la ajira kwa vijana, kwani wengi hivi sasa wameamua kujikita katika muziki wa injili kwa ajili ya kumuimbia Mungu na kujipatia kipato.
“Unapokuwa na watu wenye uzalendo kama Msama Promotions kwa hakika kabisa vijana wengi watajitokeza na watahamasika kujiingiza katika muziki huu, kwani watakuwa na uhakika wa kujipatia kipato,” alisema Mfutakamba.
Tamasha kubwa la Pasaka linatarajiwa kufanyika Aprili 24 mwaka huu siku ya sikuu ya Pasaka katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam na baadaye kufanyika mjini Shinyanga Jumatatu ya Pasaka Aprili 25 na jijini Mwanza Aprili 26, lengo lake kubwa mwaka huu ni kwa ajili ya kuwasomesha watoto yatima na kuwasiaid mtaji wa bishara