Monday, December 27, 2010

Blog :http:// kingkif.blogspot.com/



Blogger : king kif

The news with the king........

Like a true live wire , the blog throws you in the current affairs world by giving you updates on developments and issues not considered to be news at all in a straight forward language .The postings of mixed news , allows the reader to get the gist of the information without being bored .

GAZETI LA DIRA YA MTANZANIA LAINGIA MITAANI





Sunday, December 26, 2010

JK amteua Jaji Mohamed Chande Othman kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania

Rais Jakaya Mrisho Kikwete, amemteua Jaji Mohamed Chande Othman (pichani) kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania, kuanzia tarehe 28 DIsemba, 2010.

Jaji Othman anachukua nafasi ya Jaji Augustino Ramadhani anayestaafu kwa mujibu wa sheria tarehe 27 Disemba, 2010.

Kwa sasa Jaji Othman ni Jaji wa Mahakama ya Rufaa na pia ni mtaalamu binafsi juu ya hali ya Haki za Binadamu huko Kusini mwa Sudan, hadi mwezi Agosti 2011.

Jaji Othman alizaliwa tarehe 1 Januari, 1952, ana shahada ya kwanza ya Sheria (LLB) ya Chuo Kikuu cha Dar-Es-Salaam na Shahada ya Uzamili (MA) kutoka katika Chuo Kikuu cha Webster, Geneva-Uswisi.

Amewahi kuwa Makamu wa Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Rwanda huko Arusha na amewahi kushika nafasi sawa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali huko Timor Mashariki.

Jaji Othman pia, amewahi kufanya kazi ndani na nje ya nchi katika Mashirika mbalimbali ya Kitaifa na Kimataifa kama vile Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP) na Shirika la Msalaba Mwekundu.

Jaji Othman ataapishwa kesho tarehe 27 Disemba, 2010 katika viwanja vya Ikulu saa 4:00 asubuhi.

Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi
Ikulu
Dar es Salaam
26 Disemba, 2010
-----------------------

Saturday, December 25, 2010

JK in Malawi for a one Day working visit



President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete inspects a welcoming parade mounted by members of the Malawian armed forces shortly after he arrived in Blantyre’s Chileka International Airport for one day working visit.
A Malawian girl Kiki Mbilizi pins a fresh Red Rose on President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete’s coat shortly after he arrived in Blantyre for a one day working visit yesterday.
Malawi’s President Bingu wa Mutharika welcomes President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete shortly after he arrived in Blantyre for a one day working visit.
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete lays a wreath on the tomb of the former Malawi First Lady Madame Ethel Zvauya Mutharika who died on 2007 and buried at Mpumulo wa Bata Mausoleum.President Kikwete was in Malawi for a one day working visit where he held talks with his host President Bingu wa Mutharika who is also the current chairman of the African Union AU.
Malawi’s Foreign Minister Etta Banda(on her knees, right) welcomes in style, President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete shortly after he arrived in Blantyre for one day working visit yesterday. On the left is Malawi’s Minister of transport and public infrastructure. President Kikwete later held talks with President Bingu wa Mutharika of Malawi who is also the current chairman of African Union AU. The President returned to Dar es Salaam yesterday evening.

Tanesco yatangaza mgawo wa umeme nchi nzima



SHIRIKA la Umeme (Tanesco) jana lilitangaza mgawo mpya na mkubwa wa nishati hiyo ambao utavifanya viwanda, maduka, ofisi na makazi kukosa umeme kwa kati ya masaa sita hadi 12 kwa muda wa mwezi mzima.

Tangazo hilo la mgawo ambalo limekuja katika kipindi ambacho mjadala wa jenereta za kampuni ya Dowans ukiwa umeibuka tena, linatarajiwa kuongeza gharama za maisha kutokana na ukweli kuwa viwanda vingi vitalazimika kutumia jenereta katika uzalishaji licha ya Tanesco kutangaza kuwa vitapewa umeme nyakati za mchana.

Wananchi ambao kipato chao kinategemea biashara ya samaki, saluni, na vinywaji pia wataguswa na makali hayo moja kwa moja wakati mabenki, vituo vya mafuta, mahoteli na makampuni mengine ya kutoa huduma yatajikuta yakiingia gharama kubwa katika utendaji wao.

Tangazo la Tanesco limetolewa wakati kukiwa na ahadi kemkem za kumaliza kabisa tatizo la mgawo wa umeme, huku Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura) ikiwa imeliruhusu shirika hilo la umma kuongeza bei ya umeme kwa asilimia 18.5.

"Mgawo huu wa umeme umeshaanza kwenye mikoa yote na utadumu kwa majuma manne hadi katikati ya mwezi Januari mwakani," alisema meneja mawasiliano wa Tanesco, Badra Masoud alipoongea na waandishi jana.

"Mgawo utahusisha mikoa yote iliyounganishwa kwenye gridi ya taifa isipokuwa mikoa ya Ruvuma, Rukwa, Kigoma, Lindi na Mtwara."

Kwa mujibu wa Masoud, mgawo wa sasa umetokana na upungufu wa umeme uliojitokeza baada ya moja ya visima vinavyozalisha gesi vya kampuni ya Pan African Energy, kuzimwa.
Alisema kisima hicho kinachotoa gesi kimezimwa kwa ajili ya kukifanyia matengenezo ya kawaida, hivyo kusababisha upungufu wa megawati 40 za umeme zinazokwenda katika gridi ya taifa.

Pan African Energy ni kampuni ambayo inachimba gesi hiyo eneo la Songo Songo, Kilwa na baadaye husafishwa na kusafirishwa na kampuni ya Songas ambayo huzalisha umeme wa megawati 180 eneo la Ubungo na kuiuzia Tanesco.

Kwa mujibu wa makubaliano, Songas hutakiwa kuzalisha umeme kwa kiwango kilicho kwenye mkataba na ni jukumu la Tanesco kuutumia umeme huo wa gesi kulingana na mahitaji yake au kutoutumia. Tanesco huilipa Songas hata pale inapokuwa haitumii umeme wa kampuni hiyo.

Badra alisema kuwa kiwango hicho cha upungufu wa umeme kinaweza kuongezeka hadi kufikia megawati 120 jambo alilosema likitokea, shirikma hilo litazidisha mgawo.
“Wakati mwingine kunapokuwa na peak (matumizi yanakuwa makubwa), upungufu unaweza kufikia megawati 120. Ikitokea hivyo, kwa kuwa sasa tunategemea uzalishaji umeme kwa njia ya maji, itabidi nasi tuongeze mgawo,” alisema Badra.

Alieleza kuwa mgawo huo utaanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni katika baadhi ya maeneo huku maeneo yaliyopata umeme katika muda huo yakiukosa kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 5:00 usiku mara tatu kwa wiki.

Kwa mujibu wa Badra, ratiba ya mgawo huo zitatangazwa katika magazeti na vyombo vingine vya habari.
Hata hivyo, alisema baadhi ya maeneo hayatakumbwa na mgawo huo akitaja baadhi kuwa ni hospitali, pampu za maji, migodi na viwandani ambako alisema vitakosa umeme usiku ili mchana viendelee kuzalisha.

Alisema kuwa maeneo yanayopata umeme kutoka transoma ya Kipawa hawatakumbwa na mgawo huo, kutokana na kukamilika kwa matengenezo yake.

“Transfoma ya Kipawa imeshatengemaa na hivyo kuanzia Desemba 23 (jana) haki ya kupata umeme katika maeneo yaliyoathirika kutokana na kuharibika kwa transfoma hiyo, itarejea kama kawaida na wateja wa maeneo hayo hawatakumbwa na mgawo huu tulioutangaza,” alisema Badra.

Baadhi ya maeneo yanayopata umeme kutoka transfoma hilo ni pamoja na Yombo Dovya, Tandika, Temeke, Chang’ombe, Chamazi, Tazara, Maji Matitu, Charambe, Keko na Uwanja wa Taifa.

Akizungumzia siku kuu za Krisimasi na Mwaka Mpya, Badra alisema Tanesco itajitahidi kuhakikisha wananchi wanasherehekea siku hizo bila kukosa umeme huku akiwaomba radhi kwa mgawo huo.

Mgawo wa umeme, ambao ulizalisha kashfa kubwa ya Richmond ulipoibuka mwaka 2006, umeshaanza kuzoeleka kwa wananchi na ahadi za shirika hilo na wizara kugeuza tatizo hilo kuwa historia, sasa zinaonekana za kawaida.

Machi 16 mwaka huu Tanesco ilitangaza mgawo wa umeme katika mikoa yote ya Tanzania Bara uliokuwa wa saa tano kila siku. Wakati mgawo huo ukiisha, Tanesco ilitangaza kuwa tatizo la umeme sasa litakuwa historia.

Watanzania, ambao ni asilimia 12 tu wanaotumia huduma hiyo majumbani, pia walipata machungu ya mgawo wa umeme Oktoba mwaka uliopita ambapo walikosa huduma hiyo kwa saa 12 kwa siku.

Aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa shirika hilo Stephen Mabada, alitangaza mgawo huo akieleza kwamba Tanesco ililazimika kuanza mgawo huo kutokana na upungufu mkubwa wa uzalishaji umeme, uliosababishwa na kuharibika kwa mitambo minne kwenye vituo vya uzalishaji wa nishati hiyo.

Mitambo iliyoharibika ilikuwa ni ya Kidatu, mkoani Morogoro, Kihansi (Iringa) na Pangani (Tanga) wakati jijini Dar es Salaam mtambo wa kuzalisha umeme wa gesi asilia wa Songas pia uliripotiwa kuharibika.

Wakati huo, serikali iliamuru kuwashwa kwa mitambo inayozalisha umeme kwa kutumia mafuta ya IPTL licha ya kampuni hiyo na Tanesco kuwa kwenye mgogoro mkubwa ambao unashughulikiwa mahakamani.

Matatizo makubwa ya umeme yaliibuka mwaka 2006 wakati nchi ilipokumbwa na janga kubwa la ukame na ikabidi serikali ichukue hatua za dharura kumaliza tatizo hilo.

Lakini hatua hizo za dharura zikaishia kwenye kashfa kubwa ya utoaji zabuni ya uzalishaji umeme kwa kampuni ya Richmond Development LLC, ambayo ilidhihirika baadaye kuwa haikuwa na uwezo wa kutekeleza wajibu wake kwenye mkataba.

Baadaye mkataba huo ulirithishwa kwa kampuni ya Dowans Tanzania ambayo, licha ya kuchelewa, ilileta nchini mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi iliyokuwa na uwezo wa kuzalisha megawati 120.

Lakini mwaka 2008 Tanesco ilikatisha mkataba huo mwaka mmoja kabla ya kumalizika, ikidai kuwa Sheria ya Manunuzi ya Umma ilikiukwa wakati wa kuingia mkataba huo, lakini ikaahidi kuwa ina uwezo wa kuzalisha umeme bila ya kutegemea jenereta hizo.

Uamuzi huo uliifanya Dowans kufungua kesi Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Kibiashara (ICC), ikidai kuwa taratibu hazikufuatwa wakati wa kuvunja mkataba huo.

Mwaka mmoja baadaye Tanesco ikaibuka na hoja ya kutaka kuinunua mitambo hiyo ya Dowans, ikidai kuwa nchi ilikuwa hatarini kuingia kwenye tatizo kubwa la umeme na kwamba isingekuwa rahisi kununua mitambo mingine kabla ya tatizo hilo kuanza.

Hata hivyo, hoja hiyo ilipingwa vikali na Kamati ya Madini na Nishati ambayo ilieleza kuwa kununua mitambo hiyo mitumba ni kinyume na Sheria ya Manunuzi ya Umma, kitu kilichomfanya mkurugenzi wa Tanesco wa wakati huo, Dk Idris Rashid kutoa tamko kuwa iwapo nchi itaingia gizani, asilaumiwe.

Mapema mwezi huu, ICC) ilitoa hukumu ya kesi iliyofunguliwa na Dowans na kuiamuru Tanesco kuilipa kampuni hiyo binafsi fidia ya Sh185 bilioni.

Source: www.mwananchi.co.tz

Wednesday, December 22, 2010

Taarifa kwa vyombo vya Habari



Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa inafuatilia kwa ukaribu taarifa kuhusu uamuzi wa Mahakama ya Southwark mjini London, Uingereza kuiamuru Kampuni ya BAE Systems ya Uingereza kulipa faini ya Paundi za kiingereza laki tano 500,000 kwa kushindwa kuweka kumbukumbu sahihi za kihasibu kuhusu fedha zilizolipwa na kampuni ya BAE Systems kwa Mfanyabiashara Shailesh Vithlani wa Tanzania miaka mitano iliyopita.

Serikali ya Tanzania,kupitia Ubalozi wetu nchini Uingereza imeomba taarifa rasmi kutoka Serikali ya Uingereza kuhusu uamuzi huo. Serikali inasubiri kwa hamu kubwa kurejeshwa kwa bakaa ya Dola Milioni 30 za Kimarekani kama ilivyokuwa katika makubaliano kati ya Idara ya Serious Fraud (SFO) na Kampuni ya BAE Systems baada ya kuondoa faini ya kiasi cha Paundi Laki tano za Kiingereza ambazo kampuni ya BAE Systems imeamuriwa kuilipa Mahakama ya Southwark mjini London.

Mara baada ya kupata taarifa rasmi, Serikali ta Tanzania itachukua hatua muafaka ikiwa ni pamoja ni pamoja na urejeshwaji wa kiasi cha fedha kinachotakiwa kurejeshwa Tanzania kulingana na makubaliano kati ya SFO na Kampuni ya BAE Systems.

Imetolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

22 Desemba, 2010

SEKINDE KUKAMUA ZNZ 25 XMAS



Have u ever seen Devile walking naked? or Frog cross the fire? Antarakuno Sekinde ngoma ya ukae ..Daaa? Jamaa wanavamia znz tarehe 25 xmas day! Gymkana Hal... Come n see amazig! The al nite..Funika bov

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KUTOA TAARIFA ZA SIRI KATIKA
MAWASILIANO YA ELEKTRONIKI NI KOSA LA JINAI
Hivi karibuni Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imegundua kuzuka kwa tabia ya uvunjaji wa kanuni ya utunzaji wa siri za mawasiliano binafsi ya watumiaji wa huduma za mawasiliano ya simu za mkononi. Mawasiliano hayo yamefikia hatua ya kuchapishwa katika vyombo vya habari.

Mamlaka ya Mawasiliano inapenda kuchukua fursa hii kuwakumbusha wenye makampuni ya Simu na wananchi kwa ujumla kuwa, kutoa taarifa za mawasiliano binafsi ya simu bainA ya watumiaji wa huduma hiyo, ni uvunjaji wa Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta Na. 3 ya mwaka 2010 na Kanuni za Mawasiliano (Kulinda Wateja) za mwaka 2005.

Kifungu cha 98 ya Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta kinasema;

(1) “Mtu yeyote ambaye ni mfanyakazi wa kampuni yenye leseni ya kutoa huduma za mawasiliano, au mwakilishi wake, ana wajibu wa kutunza siri za mawasiliano binafsi na taarifa zozote za siri za wateja kwa mujibu wa sheria hii”

(2) “Mtu yeyote haruhusiwi kutoa taarifa binafsi za mteja yeyote alizopokea au kusikia kwa mujibu wa sheria hii isipokuwa tu mtu huyo ameruhusiwa kwa mujibu wa sheria”

Kifungu cha 123 (1) kinasema:-
Mtu yeyote ambae bila sababu za msingi atasababisha kuingilia au kuzuia kupokewa kwa mawasiliano yeyote ya kielektroniki anafanya kosa and akipatikana na makosa atatakiwa kulipa faini ya shilingi za kitanzania zisizopungua milioni tano au kwenda jela kwa muda wa usiopungua miaka miwili au adhabu zote kwa pamoja”

Kanuni ya 12 ya Kanuni za Mawasiliano
za mwaka 2005 za Tanzania (Kulinda Wateja) inasema:-

“Mtoa huduma za Mawasiliano haruhusiwa kuingilia kati, kusikiliza au kutoa taarifa zozote za mazungumzo ya mteja yeyote yaliyopitia kwenye mtandao wa mtoa huduma, isipokuwa kwa ruhusa kulingana na mahitaji maalumu kwa mujibu wa sheria zilizopo”

Kutolewa kwa taarifa za mawasiliano binafsi ya watumiaji wa simu za mkononi ni lazima kunafanywa na mtu mwenye ujuzi na uelewa wa jinsi ya kupata taarifa hizo na wenye ruhusa ya kufanya hivyo katika mtandao wa Kampuni husika ya kutoa huduma ya mawasiliano; ama peke yake au kwa kushirikiana na wenzake kwa kuingia kwenye mtandao kwa makusudi kwa lengo la kuingilia mawasiliano binafsi ya watu, ambayo ni uvunjaji na kinyume na matakwa ya kifungu cha 123 cha Sheria Na. 3 ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta.

Mamlaka ya Mawasiliano inayakumbusha Makampuni ya simu kuweka uzuizi na kuhakikisha siri za mazungumzo binafsi ya wateja zinahifadhiwa na hazitolewi kwa yeyote isipokuwa kwa mujibu wa sheria na; kuhakikisha yanafanya uchunguzi kugundua walioiningilia mazungumzo binafsi ya wateja.

Wananchi wanapewa tahadhari kuhusu kutafuta au kutaka kupata taarifa za mawasiliano ya siri kutoka kwa watoa huduma na kuzitumia taarifa hizo binafsi za mawasiliano pasipo kufuata utaratibu ulioruhusiwa kisheria.

Kwa taarifa ambazo zimechapishwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari hivi karibuni, Mamlaka ya Mawasiliano inafanya uchunguzi wa uvunjwaji huo wa sheria kwa kutoa taarifa binafsi za wateja kinyume na sheria. Baada ya kuwabaini wahusika, Mamlaka itachukua hatua za sheria kwa yeyote atakayebainika kuvunja sheria hiyo.

Imetolewa na
Mkurugenzi Mkuu
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)
22 Desemba 2010

Tuesday, December 21, 2010

ZIFF MIN-FESTIVAL at NGOME KONGWE - ZANZIBAR



Habari,

Ndugu zetu wadau wa kiwanda cha filamu Tanzania, Zanzibar International Film Festival (ZIFF) inapenda kuwataarifu kuwepo kwa ZIFF Min-Festival itakayofanyika Ngome Kongwe, Zanzibar kuanzia tarehe 31/12/2010 hadi 2/01/2011, itakua ni Tamasha dogo la siku 3 katika kutoa muamko kwa Tamasha kubwa la ZIFF lijalo (2-10 Julai, 2011).

Tamasha hili dogo litajumuisha filamu za kitanzania peke yake ili kuendelea kutoa mwamko kwa watengenezaji filamu wa Tanzania kufanya vyema katika tasnia hii, Tamasha hili litaonesha filamu 6 za Kitanzania na filamu 2 bora kati ya hizo zitaenda kuoneshwa katika Tamasha kubwa la filamu Afrika - FESPACO huko Burkina Faso.

Kama ilivyo ada ya Tamasha la Filamu la Nchi za Majahazi, tutakua pia na makundi ya muziki na wakati huu kundi zima la THT litafanya maonesho kwa siku zote tatu, watakao kuwepo ni Mwasiti, Marlaw, Mataluma, Amin, Barnaba, Pipi, THT Dancers na wengineo. Kwa habari zaidi tembelea www.ziff.or.tz

Tunapenda kuwakaribisha wadau wote na waandishi wa habari katika mkutano wa waandishi wa habari utakaofanyika katika ukumbi wa Habari - Maelezo, Dar es Salaam, kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 5 asubuhi kesho Jumatano, tarehe 22/12/2010

Ahsanteni!

Daniel Nyalusi
Festival Manager
Zanzibar International film Festival

Serikali kuendelea kuwatumia Wastaafu kwa huduma za Ushauri


Katibu Mkuu Kiongozi, Bw. Philemon Luhanjo

Umetolewa mwito kwa wastaafu wa utumishi wa umma kwenye ngazi za uongozi, kuendelea kuutumikia umma katika ngazi ya ushauri, kufuatia uzoefu wao wa muda mrefu kwenye utumishi wa umma, hivyo kubakia na uwezo wa kuona zaidi kuliko watumishi wanao waachia uongozi.

Mwito huo, umetolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Bw. Philemon Luhanjo, wakati wa hafla ya kumuaga Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bibi Thecla Shangali, pamoja na wastaafu wengine wa tume hiyo, iliyofanyia jana usiku kwenye ukumbi wa Paradise City Club, hapa jijini Dar es Salaam.

Bwana Luhanjo amesema, wastaafu wa utumishi wa umma ni hazina kubwa sana kwa taifa na ujuzi wao na uzoefu wao bado unahitajika sana katika ngazi ya ushauri, hivyo amewashauri viongozi wa utumishi wa umma walio madarakani, kuhakikisha wanaitumia hazina hii, kwa kuwatumia wastafu wao kwa huduma za ushauri, ‘consultancy’ kila watakapo ona hali inaruhusu.

Kwa upande wao, Katibu Mstaafu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bibi Thecla Shangali, akizungumza kwa niaba ya wastaafu wenzake, alisisitiza kuwa tayari wakati wowote, kuendelea kuipa Tume ya Utumishi, ushauri wake kila atakapohitajika.

Bibi Shangali, ambae ametumikia utumishi wa umma wa takriban miaka 40, ameasema utumishi wa umma, unakabiliwa na changamoto mbalimbali na kuelezea moja ya changamoto kubwa za watumishi wa umma, ni maslahi duni, ukilinganisha na sekta binafsi.

Amewasisitiza watumishi wa umma, kuongeza bidii katika utendaji wao wa kazi, ili kuleta tija zaidi katika maeneo yao, itakayoongeza mapato ya serikali na kuijengea serikali uwezo wa kuboresha zaidi maslahi yao.

Pamoja na changamoto hiza za maslahi duni serikalini, Bibi Shangali, ameisifu serikali kuwa ndiye mwajiri bora zaidi kwa ajira yenye uhakika (job security),na mwenye mazingira bora kabisa ya kufanyia kazi, (working envirionment), vitu vinavyosababisha watumishi wa umma kufanya kazi kwa moyo wa kujitolea (job satisfaction) na hivyo wengi hata walio kwenye sekta binasfi, kutamani kupata kazi serikalini.

Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Jovin Kitambi, alimpongeza Bibi Shangali kwa utumishi uliotukuka wakati Kaimu Katibu wa Tume hiyo, Bw. Donald Ndagula akiahidi kuyaenzi mazuri yote yaliyofanywa na Bi. Shangali, ambaye ndiye muasisi wa Tume hiyo iliyoundwa upya kwa sheria mpya ya Utumishi wa Umma, number 8 ya mwaka 2002.

Sunday, December 19, 2010

GAZETI LA DIRA YA MTANZANIA LEO





RAIS JAKAYA KIKWETE NA BALOZI CARLTON WAZINDUA HOTEL YA MOUMT MERU.

President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete cuts the tape to officially re-open Mount Meru Hotel in Arusha yesterday evening. Flanking the president on the left is the new investor for Mount Meru Hotel, the Chairman of HODI Hotels Ambassador Carlton Masters. Third Left is the Minister for Natural Resources and Tourism Ezekiel Maige and on the right is Arusha Regional Commissioner Isidori Shirima.
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete unveils a plaque to signal the official re-opening of the Mount Meru Hotel in Arusha yesterday evening. On the left is the new investor for the Hotel ambassador Carlton Masters who is also the Chariman of Hodi Hotels and Vice Chairman of South African Development Enterprise Fund) SADEF.

President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete addresses invited guests and dignitaries who attended the re-opening of Mount Meru hotel in Arusha yesterday evening

The Chairman of Hodi Hotels Ambassador Carlton Masters guides President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete to the newly refurbished boardroom at the re-opened Mount Meru Hotel in Arusha yesterday evening.(Photos by Freddy Maro).

Thursday, December 16, 2010

JK Awaapisha Makatibu Tawala




Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete jana amewaapisha Makatibu tawala wapya wa mikoa sita katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Makatibu Tawala hao wapya walioapa jana mbele ya Rais ni pamoja na Bi.Evelyne Philbert Itanisa wa mkoa wa Arusha, Benedict Ole Kuyan wa Mkoa wa Tanga,Mgeni Sufiani Baruani wa Mkoa wa Morogoro na Liana Ayoub Hassan wa Singida.Wengine ni Nassor Mohamed Mnambila wa Kagera na Kudra Juma Mwinyimvua wa Tabora.Pichani Katibu Tawala mpya wa mkoa wa Arusha Bi.Evelyne Philbert Itanisa akila kiapo mbele ya Rais Dr.Jakaya Kikwete .

Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi miongozo ya kazi Katibu Tawala Mpya wa mkoa wa Arusha Evelyne Itanisa baada ya kula kiapo katika hafla iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam jana jioni.(Picha: Freddy Maro).

Monday, December 13, 2010

Mabalozi wa Sweden na Norway wawasilisha hati za utambulisho kwa Rais Kikwete


Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo amepokea hati za utambulisho kutoka kwa Mabalozi wa Sweden na Norway katika hafla fupi iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam.Waliowasilisha hati zao ni Balozi Lennarth Hjelmaker wa Sweden na Balozi Bi.Ingunn Klepsvik wa Norway.Pichani Balozi Ingunn Klepsvik wa Norway akiwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete.
Picha na Freddy Maro - Ikulu

DIRA YA MTANZANIA JUMATATU WIKI HII




Profesa Nyang'oro aeleza sababu za kuandika kitabu cha JK



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akitia saini kitabu cha wasifu nakala ya Mama Salma Kikwete wakati wa uzinduzi wa kitabu hicho. Profesa Julius Nyang'oro (pichani katikati) ndiye mwandishi wa kitabu hicho.

Rais Kikwete akiwa kwenye picha ya pamoja na marafiki wa Profesa Nyang'oro wakati wa uzinduzi wa kitabu chake cha wasifu wa JK. Profesa Nyang'oro anafundisha Sayansi ya Siasa kwenye Chuo Cha North Carolina nchini Marekani.

Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;

Mheshimiwa Mohammed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;

Mheshimiwa Mizengo Pinda, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;

Viongozi wa Serikali, Waalikwa, Mabibi na Mabwana;



Ni furaha kubwa kwangu kuweza kushiriki katika uzinduzi wa majuzuu mawili ya kitabu juu ya Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kabla ya yote, napenda kutumia fursa hii kumpongeza Rais kwa ushindi wake wakati wa uchaguzi mkuu uliofanyika hivi karibuni. Kutokana na raghba yangu ya kitaaluma na raghba ya kufanya utafiti juu yake, nilifuatilia uchaguzi huo kwa karibu na ninakiri kwamba nilivutiwa na ushupavu wake alipokuwa anasafiri sehemu mbalimbali za nchi, akiomba kura. Siku ya kuhitimisha kampeni kwenye Viwanja vya Jangwani, nilikuwa miongoni mwa waliohudhuriwa na nilivutiwa sana alipotaja maelfu ya kilomita alizosafiri wakati wa kampeni, mamia ya saa alizotumia angani akieleza kwa nini anataka kuchaguliwa tena na mamia ya hotuba alizotoa. Hongera sana Mheshimiwa.

Aidha, nawatakia wote siku njema ya kusherehekea Uhuru.

Kitabu hiki ni matokeo ya mradi uliochukua miaka mitatu. Namshukuru Rais kwa kukubali ombi langu la kumhoji mara kadhaa, mbali na ratiba yake nzito. Natoa shukrani za pekee kwa wasaidizi wake kadhaa ambao walikuwa muhimu sana katika kuandaa mahojiano na kwa kuandaa uziunduzi huu wa kitabu.

Aidha, natoa shukrani za pekee kwa Profesa Imani Swilla kwa kushiriki katika mradi huu. Yeye aliandaa tafsiri ya Kiswahili ya kitabu hiki. Napenda pia kumshukuru Profesa Severine Rugumamu kwa kukubali kutoa tathmini na maoni juu ya kitabu hiki wakati huu wa uzinduzi. Lakini, napenda kusema kwamba kama mwandishi wa kitabu hiki, nawajibika kwa mapungufu yoyote yaliyomo kwenye kitabu.

Nathamini sana mradi huu kwa sababu kadhaa. Wazo la kuandika kitabu juu ya JK liliniijia kwa mara ya kwanza nilipotambua kwamba hakuna wasifu mkubwa wowote ulioandikwa juu ya rais wa Tanzania tangu wasifu wa Mwalimu Julius Nyerere ulioandikwa na William E. Smith mwaka 1971. Kwa hiyo, niliamua kuanza kuziba pengo lililopo kwa kufanya utafiti juu ya JK. Ingawa William E. Smith alifanya kazi nzuri sana alipoandika wasifu wa Mwalimu, mara nyingi nilisumbuliwa na kitu kimoja: Smith siyo Mtanzania. Niliwaza kuwa kuna watu wengi nchini ambao, kama Smith, wanaweza kuandika vizuri juu ya viongozi wetu. Ndiyo maana niliamua kuandika juu ya wasifu wa JK.

Uamuzi wa kuandika juu ya JK ulisukumwa na sababu nyingine binafsi. Ingawa JK ananizidi kidogo umri, yeye ni rais ambaye kisaikolojia ninahusiana naye kwa sababu tumeishi katika vipindi vinavyofanana na tumekua katika miaka ya 1960, 1970 na 1980.

Nilipofuatilia mabadiliko na maendeleo yake kama mtu, mwanasiasa na mtumishi wa umma, nilikumbuka mambo mengi ambayo mimi mwenyewe niliyapitia nyakati hizo, kwa mfano: matembezi marefu ya kuunga mkono Azimio la Arusha mwaka 1967. Ingawa nilikuwa mdogo mno kuweza kushiriki kwenye matembezi hayo, nakumbuka baadhi ya watu niliosoma nao ambao walitembea mamia ya maili kwenda Dar es Salaam kumpongeza Mwalimu juu ya Azimio la Arusha; Mwongozo wa 1971; Jeshi la Kujenga Taifa ambapo nilikutana na watu ambao wamekuwa ni rafiki wa kudumu; Azimio la Musoma la 1975; mchango wa Tanzania katika ukombozi wa kusini mwa Afrika; kuingia madarakani kwa Rais Ali Hassan Mwinyi na mwishowe, kurudishwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 na kuchaguliwa kwa Rais Mkapa mwaka 1995.

Hatimaye, ushindi wa JK kwenye uchaguzi wa rais wa mwaka 2005 uliokuwa wa kishindo. Ni nadra ulimwenguni kote kwa mgombea wa chama kilichopo madarakani kushinda kwa idadi aliyoshinda JK: zaidi ya asilimia 80 ya wapiga kura walimchagua kuwa Rais wa Tanzania. Kama mwanataaluma wa siasa, nilivutiwa sana na ushindi wa JK, ulioelezwa wakati huo kuwa ushindi wa tsunami.

Matukio yote haya yalikuwa muhimu sana katika historia ya siasa ya nchi yetu. Nilipokuwa naandika juu ya matukio haya kuhusiana na mabadiliko na maendeleo ya JK kama kiongozi, nilikumbuka mambo mengi ambayo ni vigumu mtu kuelewa kama hakuyapitia. Changamoto kubwa kwangu kama mwanataaluma ilikuwa ni kutofautisha kumbukumbu zangu na tathmini halisi ya vipindi hivyo. Katika maisha, naelewa kwamba huwezi ukachunguza kitu bila kuwa na maoni yako. Ni wazi kwamba uelewa wangu wa siasa za Tanzania unatokana na matukio hayo niliyoshiriki. Lakini ni matumaini yangu kwamba uchambuzi wangu wa vipindi mbalimbali katika kitabu hiki unaonyesha uelewa wangu wa Tanzania, bila kuathiri uchambuzi wangu wa kitaaluma.

Moja ya sababu kubwa ya utafiti wangu juu ya JK ni kwamba naona kuwa urais na uongozi wake umekuja wakati nchi inakabiliana na changamoto kubwa. JK ni rais wa kwanza wa Tanzania ambaye hakushiriki katika mapambano ya kupata uhuru. Alikuwa na umri wa miaka 12 Tanganyika ilipopata uhuru. Vipindi vya urais wa Mwalimu, Mzee Mwinyi na Mzee Mkapa vilikuwa ni vipindi vya kuimarisha uzalendo na uhuru.

Changamoto za vipindi vya mwanzo ni tofauti na zile ambazo zinaukabili urais na uongozi wa JK. Ingawa moja ya changamoto ya JK ni kuimarisha mshikamo wa kitaifa, lakini changamoto muhimu zaidi kwa wakati huu ni kuleta maendeleo ya uchumi, kwenye mazingira magumu zaidi ya mfumo wa uchumi wa ulimwengu. Mfano mzuri wa swala hili ni kuhusu hali ya vijana wa nchi hii. Ni wazi kwamba vijana ni kundi muhimu sana, ukizingatia ukweli wa masuala ya idadi ya watu nchini.

JK atakuwa mtu wa kwanza kukiri kwamba ni vigumu kumaliza kiu ya ajira ya vijana, elimu yao na masuala mengine. Yeye mwenyewe alisaidia katika kuikuza kiu hii wakati wa kampeni za urais za mwaka 1995 na 2005. Wakati wa kampeni zote mbili, aliyapa umuhimu zaidi maslahi ya vijana.

Aidha, changamoto anazokumbana nazo JK ni ngumu zaidi kuliko za waliomtangulia kwa sababu ya mabadiliko ya kiteknolojia ambayo yamwezesha kila mtu, hata vijijini, kupata taarifa juu ya maendeleo ya kitaifa na matukio ulimwenguni. Kwa hiyo, kila wakati, utendaji wake unalinganishwa na utendaji wa viongozi ulimwenguni kote. Hii ni changamoto kubwa kwa rais.

JK kama kiongozi anapaswa kuelewa matarajio ya wananchi na hapana shaka kwamba anaelewa. Nilipokuwa naandaa kitabu hiki na kumfuata wakati wa baadhi ya ziara zake mikoani, nilielewa kwamba anaelewa fika changamoto hizi na anaweza kukabiliana nazo. Aliwasiliana vizuri na watu aliokutana nao na alioenekana kuelewa changamoto zao za kila siku. Hii inaeleweka kwa sababu yeye mwenyewe alikulia katika mazingira ya kawaida na anaelewa vizuri maisha ya kila siku ya watu wa kawaida. Namtakia mema na kila la heri katika jitihada zake kwa sababu mafanikio yake yataboresha hali ya kiuchumi na kijamii ya wananchi.



Kama wote mnavyojua, kuandika kitabu ni jambo lenye upweke sana. Mradi huu haukuwa tofauti. Mradi kama huu unahitaji muda, umakini, tafakari na uvumilivu. Nilipitia yote haya. Lakini najua kwamba nisingeweza kufanikisha mradi huu bila familia yangu kujitoa: mke wangu Alu na watoto wetu Alma na Yusuf. Walivumilia kutokuwepo kwangu kwa mara nyingi, wakati nikifanya utafiti wa kitabu hiki. Nawashukuru sana kwa kuelewa hali hii. Kwa njia moja au nyingine, wao walinitia moyo na kunihimiza kumaliza kitabu. Kwa hiyo, kitabu hiki nimekiandika kwa heshima yao na kwa heshima ya wazazi wangu ambao mapenzi yao yamekuwa ni faraja kubwa kwangu siku zote.

Napenda pia kuwashukuru marafiki zangu wengi, baadhi yao ambao wapo hapa leo, kwa kuniunga mkono na kunitia moyo wakati nikiandika. Nimewataja baadhi yao kwenye kitabu kwa sababu tumeshirikiana mambo mengi kwenye maisha na kwa sehemu kubwa, tulifurahia mambo mengi hayo.

Bila kutaja majina, nawashukuru watu wengi ambao niliwahoji na baadhi yao wapo hapa nasi. Ni matumaini yangu kwamba tafsiri ya matukio tuliojadili yanalingana na uchambuzi wenu mliofanya nilipowahoji.

Africa World Press, mchapishaji wa kitabu hiki, alifanya kazi nzuri sana kwa kukitoa kitabu katika muda mfupi sana na kushughulikia masuala yote ya itifaki na kitaalamu. Napenda pia kulishukuru Duka la Vitabu la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kukubali kuwa msambazaji pekee wa kitabu nchini. Najua ni jukumu kubwa sana lakini naamini kwamba watafanya kazi nzuri.

Kwa kuhitimisha, napenda kwa mara nyingine, kumshukuru Rais kwa kunipatia muda wakati nafanya utafiti. Kama nilivyosema kwenye utangulizi wa kitabu, hili ni juzuu la kwanza la mradi wangu. Tayari nimeanza kufanya uchambuzi makini wa matokeo ya sera zake kwa ajili ya hatua nyingine ya mradi huu. Naamini kwamba wote mnanitakia mema katika jitihada zangu, kwa sababu kama nilivyosema mwanzoni mwa hotuba hii, tunahitaji aina hii ya utafiti ili kuhifadhi historia ya nchi yetu.

Ni matumaini yangu kuwa watu watapata muda wa kusoma kitabu tunachozindua leo. Nimerahisisha suala zima kwa kutayarisha matoleo ya Kiswahili na Kiingereza ya kitabu hiki. Lililobaki ni kwenu kukisoma.

Asanteni sana.

Sunday, December 12, 2010

EXCLUSIVE: DR. REMY HATUNAE TENA!

Watanzania wote wamepatwa na simanzi baada ya usiku wa kuamkia leo mwanamuziki mkongwe na mahiri Dk. Remy Ongala kufariki dunia.

GAZETI LADIRA LIPO MTAANI LEO HII. PATA NAKALA YAKO MAPEMA.


Kama kawaida gazeti lako la kila wiki linalotolewa na DIRA MEDIA GROUP leo lipo mtaani kwa tsh. 400/- pata nakala yako upate kujua kinachoendelea ndani ya nchi yako na hata nje ya nchi kupitia waandishi waliobobea katika kuandika habari za kiuchunguzi na zenye uhakika. ndani ya gazeti la DIRA utapata habari za kisiasa, kiuchumi, kijamii, michezo na burudani.

Saturday, December 11, 2010

KITABU CHA JK CHAZINDULIWA





Baadhi ya wanafamilia ya Mheshimiwa Rais Kikwete wakiperuzi kurasa za kitabu cha Wasifu wa JK kilichozinduliwa leo Ikulu Dar es salaam.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Bwana Beno Malisa akizungumza na Miraji Kikwete kwenye uzinduzi wa Kitabu Cha Wasifu wa JK Ikulu jijini Dar es salaam.
Nakala ya kiingereza ya Kitabu cha Wasifu wa JK kama kinavyoonekana. Picha ya chini ni Profesa Nyang'oro akitia saini nakala za kitabu hicho zilizogaiwa bure kwa wageni wote waalikwa waliofika kwenye hafla hiyo. Vitabu hivyo vitaanza kuuzwa kwenye duka la vitabu la Chuo Kikuu Cha Dar es salaam kuanzia kesho tarehe 10-12-2010 kwa gharama ya shillingi 25,000/=

Monday, December 6, 2010

WEB YA MAHAKAMA YA TANZANIA


Hili ndilo libeneke la mahakama ya rufaa lililozinduliwa
leo na Makamu wa Rais Dk. Mohamed Ghalib Bilali jijini Dar es salaam.

THE BEN TV DIPLOMATIC AWARDS 2010



BEN TELEVISION

25 ASHLEY ROAD

TOTTENHAM

LONDON, N17 9LJ


Monday 6th December 2010

The Ben TV Diplomatic Awards recognises the international and continental achievements made over the past year by our continent at home and in the Diaspora within the diplomatic community. Playing host to the first sub-Saharan World Cup, defusing political and regional tensions, and continuing the fight for awareness of our causes, our high commissions and embassies have been pivotal to the casting off the dark shadows that have engulfed Mother Africa. For all this and more, as the first black ethnic station broadcasting in Europe, we give them a night that we know will serve their reputation for years to come.

We cannot leave out the achievements made through the Caribbean and Asia. Much investment has been provided from these regions into Africa, to our continuous development. Alongside their own setbacks, the Caribbean and Asia have united their Diasporas and home-bases to build representative and efficient embassies which represent their own development.

In these circumstances, Ben TV will be awarding members of the diplomatic community from Africa, the Caribbean and Pacific in recognition of the contribution awards in the following categories:

· Diaspora growth, development and involvement

· Good customer service at the High commission/embassy

· Promoting country’s image abroad

· Country’s Human Development

Other winners are:

AFRICA CATEGORY- Nigeria, Uganda, Kenya, Morocco, Namibia, Lesotho, Gambia, Tanzania Equatorial Guinea, South Africa, Ghana, Mozambique, Swaziland

CARIBBEAN/ASIA/PASIFIC CATEGORY: India, Fiji, New Zealand ,Australia, Trinidad and Tobago, St. Lucia, Jamaica, St Kitts, Barbados

Other categories to be won are:

Diplomat of the year from Africa, Caribbean and Pacific 2010

Diplomat of the Year from the Americas

Deputy Head of mission of the year

Distinguished contribution to diplomacy

The BEN TV DIPLOMATIC AWARDS will be adding glamour to Africa’s Golden Jubilee celebrations with:

* Top Nollywood stars & the best of African film stars

* UK celebrities and crème de la crème

* Diplomats and professionals

Come and experience spectacular out-of-Africa entertainment, an evening of parade of stars, awards ceremony, glamour, live performances from your favourite film stars, comedy, dance, cultural entertainment, food and music.

18th December 2010

29 The Broadway Stratford, London, E15 4BQ

Time: 6pm prompt to 2am.

Signed.

Ayoub mzee

Public/current Affairs Desk

BEN TV SKY 184

Kindly advice BEN TV Events Manager, Merissa and Miski on 02088088800 or Ayoub mzee on 07960811614 For further information: email swahilidiaries@yahoo.co.uk or marketinge@bentelevision.com.

Signed.

Ayoub mzee

Public/current Affairs Desk

BEN TV SKY 184

Notes

Africa is truly a great nation with great people. We celebrate Africa at 50. We celebrate you and other great people like you as an inspiration to the next generation of leaders.

Whilst this is expected to be a self sponsored event, kindly note that we would welcome any sponsorship contribution you may offer to make this event successful or if you have a large contingent of guests, you may want to reserve separate table(s).

BEN TV is a Black and ethnic oriented ,urban , diverse and cosmopolitan Family channel ,established to provide a whole some mix of entertainment ,educative and informational programmes suitable for family viewing .It also includes a range of cultured programming to empower ,transform and challenge the conventional perception of Africa, Caribbean and African Diaspora.

JK And Tvangirai







President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete meets Zimbabwean Prime Minister Morgan Tvangirai in Brussels yesterday.
( Photos: Freddy Maro)

Wednesday, December 1, 2010

World AIDS Day 2010: Universal Access and Human Rights



Statement by Thoraya Ahmed Obaid,
UNFPA Executive Director, 1 December 2010

Today, on World AIDS Day, we call for universal access and human rights for all and we extend solidarity to all people living with HIV.

UNFPA welcomes the new data from UNAIDS showing that the epidemic is changing course, thanks to bold and concerted actions, including an emphasis on the right to prevention, treatment, care and support.

New HIV infections have fallen by nearly 20 per cent in the last 10 years, AIDS-related deaths are down by nearly 20 per cent in the last five years, and the total number of people living with HIV is stabilizing.

We are coming closer to a world where no children have to grow up with the burden of HIV as more and more babies are protected from mother-to-child transmission of the virus.

Moreover, we applaud the leadership of young people, who have adopted safer sexual practices and are now leading the prevention revolution. Among young people in 15 of the most severely affected countries, the rate of new HIV infections has fallen by more than 25 per cent.

We now have more reason than ever to dream of a world with zero new HIV infections, zero AIDS-related deaths, and zero discrimination. Now is the time to build on the successes we have had because too many women and young people still lack access to the information and services they need to protect themselves.

By further integrating HIV programmes and services with sexual and reproductive health, we can make the response even more effective.

UNFPA is working in partnership with other UN agencies, governments, civil society and private sector to promote universal access to prevention, treatment, care and support, and respect for human rights for all.

We will continue to share, care and dare to do the right thing and stand up for the principles of human rights, especially for the most vulnerable and most at risk populations.

Today, and every day, let us join hands to make universal access and human rights come true for everyone.