Saturday, November 6, 2010

MATUKIO YA KUAPISHWA KWA RAIS LEO





Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Davis Mwamunyange wakiingia Uwanja wa Uhuru kabla ya kuapishwa leo mchana.

Rais wa Afrika ya Kusini Mhe. Jacob Zuma akiwasili uwaja wa Uhuru leo kushuhudia kuapishwa kwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo.

Baadhi ya wakuu wa nchi za Afrika waliohudhuria sherehe hizo za kuapishwa leo mchana


Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameapishwa leo majira ya saa tano na nusu asubuhi baada ya kushinda matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31, 2010.

Rais Kikwete ameapa mbele ya jopo la viongozi wa serikali wakiwemo Jaji Mkuu, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Katibu Mkuu Kiongozi, Jopo la Majaji, Wakuu wa Vyombo vya ulinzi, Viongozi Watatu wa Madhehebu ya Dini, Wazee Wawili kutoka Tanzania Bara na Tanzania Visiwani na Karani wa Baraza la Mawaziri.
Baada ya kuapishwa, Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete alikaa kwenye kiti cha jadi na kukabidhiwa Mkuki na Ngao na wazee wa jadi kama ishara ya uongozi na mafanikio mema.
Naye Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mohamed Gharib Bilal aliapishwa mara baada ya Mheshimiwa Rais kumaliza kiapo chake.
Baada ya dua na sala kutoka kwa viongozi wa dini na madhehebu ya dini, Mheshimiwa Rais Kikwete anategemewa kupokea salamu ya Heshima kutoka kwa majeshi ambapo mizinga 21 itapigwa, bendera ya Rais itapandishwa, gwaride litaunda Umbo la Alpha na hatimaye Rais atakagua gwaride hilo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kuhutubia wananchi wa Tanzania kutokea hapa Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.
Sherehe hizi za kuapishwa rasmi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete zimehudhuriwa na marais watano wa nchi za Afrika akiwemo Mhe. Robert Mugabe wa Zimbabwe, Mhe. Mwai Kibaki wa Kenya, Mhe. Jacob Zuma wa Afrika ya Kusini, Mhe. Rupia Banda wa Zambia na Mhe. Joseph Kabila wa DRC.
Nao Umoja wa Afrika umewakilishwa na Mhe. Jean Ping ambaye ni Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika.

Chanzo ni
http://mawasilianoikulu.blogspot.com

Friday, October 29, 2010

Rais Kikwete akutana na viongozi wa dini Ikulu Dar es Salam


Viongozi wa dini wakiwa katika picha ya pamoja na Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete wakati walipokutana na kufanya mazungumzo ikulu jijini Dar es Salaam leo jioni
(Picha na Freddy Maro).

WASIFU WA DR SLAA



Dk Slaa alizaliwa Oktoba 29, mwaka 1948 wilayani Karatu. Alipata elimu ya msingi katika shule za Karatu na Kwermusi (Mbulu) kati ya mwaka 1958 na 1965.

Alisoma elimu ya sekondari katika Shule za Dung’unyi Seminari na Itega Seminari kati ya mwaka 1966 na 1971.

Ni kiongozi mwenye stashahada tatu pamoja na shahada ya Uzamivu (PhD). Anayo Shahada ya Uzamivu (PhD ) katika Sheria ya kanisa kutoka Chuo Kikuu cha St. Urban, Rome. Pia anastashahada ya Theolojia kutoka Kipalapala Seminari, Stashahada ya falsafa kutoka Kibosho Seminari, Stashahada ya Afya ya Macho kutoka Kituo cha Kimataifa cha Macho.

Amewahi kuwa padri wa Kanisa Katoliki kuanzia mwaka 1977 hadi 1991, akishika nafasi za kiutawala katika kanisa pia. Amepata kuandika vitabu vitatu ambavyo ni Utimilifu wa Msichana (1977), Utimilifu wa Mvulana (1977) na Expediency and exigency Liturgical Legislation (1981). Ni mzungumzaji wa Lugha nane kwa ufasaha; ambazo ni Kiswahili, Kiingereza, Kilatini, Kiitaliano, Kijerumani, Kihispania, Kireno na Kifaransa.

FOR IMMEDIATE RELEASE



Model casting on Monday November 1st at Southern Sun Hotel from 1pm until 3pm.

Are you a Model? Or perhaps you aspire to be one?

Men and Women; All are welcome to audition for the chance of being a part of Swahili Fashion Week 2010.

Southern Sun Hotel will be hosting the third Swahili Fashion week model casting at 1pm on the 1st of November. Our aim is to offer this opportunity to all people who aspire to be a model. Anyone with the dream of becoming a model has the opportunity to audition for the biggest fashion filled event of the year.

Swahili Fashion week is a platform for designers – both fashion and accessory – from Swahili speaking countries to showcase their creativity, market their art and network with their clientele. This is all aimed at promoting fashion as an income generating, job creating industry while emphasizing a “Made in East Africa” concept.

Swahili Fashion Week 2010 has been sponsored by the home of Swahili Fashion Week - Southern Sun, Origin Africa, USAID Compete, MALARIA HAIKUBALIKI , BASATA (Baraza La Sanaa Taifa), Ultimate Security, Monier 2000, Colour Print Ltd, Global Outdoor Ltd, Amarula, Vayle Springs Ltd, ZG Films, Darling Hair, Danish make up designs, Nipashe, Bilicanas, Perfect Machinery Ltd, 1&1 Internet Solutions, Sengi Tours, Ifashion, 361 Degrees and EATV & East Africa Radio.