Friday, October 29, 2010

Rais Kikwete akutana na viongozi wa dini Ikulu Dar es Salam


Viongozi wa dini wakiwa katika picha ya pamoja na Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete wakati walipokutana na kufanya mazungumzo ikulu jijini Dar es Salaam leo jioni
(Picha na Freddy Maro).

WASIFU WA DR SLAA



Dk Slaa alizaliwa Oktoba 29, mwaka 1948 wilayani Karatu. Alipata elimu ya msingi katika shule za Karatu na Kwermusi (Mbulu) kati ya mwaka 1958 na 1965.

Alisoma elimu ya sekondari katika Shule za Dung’unyi Seminari na Itega Seminari kati ya mwaka 1966 na 1971.

Ni kiongozi mwenye stashahada tatu pamoja na shahada ya Uzamivu (PhD). Anayo Shahada ya Uzamivu (PhD ) katika Sheria ya kanisa kutoka Chuo Kikuu cha St. Urban, Rome. Pia anastashahada ya Theolojia kutoka Kipalapala Seminari, Stashahada ya falsafa kutoka Kibosho Seminari, Stashahada ya Afya ya Macho kutoka Kituo cha Kimataifa cha Macho.

Amewahi kuwa padri wa Kanisa Katoliki kuanzia mwaka 1977 hadi 1991, akishika nafasi za kiutawala katika kanisa pia. Amepata kuandika vitabu vitatu ambavyo ni Utimilifu wa Msichana (1977), Utimilifu wa Mvulana (1977) na Expediency and exigency Liturgical Legislation (1981). Ni mzungumzaji wa Lugha nane kwa ufasaha; ambazo ni Kiswahili, Kiingereza, Kilatini, Kiitaliano, Kijerumani, Kihispania, Kireno na Kifaransa.

FOR IMMEDIATE RELEASE



Model casting on Monday November 1st at Southern Sun Hotel from 1pm until 3pm.

Are you a Model? Or perhaps you aspire to be one?

Men and Women; All are welcome to audition for the chance of being a part of Swahili Fashion Week 2010.

Southern Sun Hotel will be hosting the third Swahili Fashion week model casting at 1pm on the 1st of November. Our aim is to offer this opportunity to all people who aspire to be a model. Anyone with the dream of becoming a model has the opportunity to audition for the biggest fashion filled event of the year.

Swahili Fashion week is a platform for designers – both fashion and accessory – from Swahili speaking countries to showcase their creativity, market their art and network with their clientele. This is all aimed at promoting fashion as an income generating, job creating industry while emphasizing a “Made in East Africa” concept.

Swahili Fashion Week 2010 has been sponsored by the home of Swahili Fashion Week - Southern Sun, Origin Africa, USAID Compete, MALARIA HAIKUBALIKI , BASATA (Baraza La Sanaa Taifa), Ultimate Security, Monier 2000, Colour Print Ltd, Global Outdoor Ltd, Amarula, Vayle Springs Ltd, ZG Films, Darling Hair, Danish make up designs, Nipashe, Bilicanas, Perfect Machinery Ltd, 1&1 Internet Solutions, Sengi Tours, Ifashion, 361 Degrees and EATV & East Africa Radio.

Sunday, October 10, 2010

GAZETI LA DIRA YA MTANZANIA WIKI HII







NYUMBA HII INAUZWA ....

DIRA YA MTAZANIA ...

Diamond kwenda Uingereza




Salam,

Urban Pulse Creative ikishirikiana na Aset Inapenda kuwataarifu wadau wote wa Music wa bongo Flava na Hip Hop kuwa imeandaa tamasha maalum linaloitwa URBAN TOUR ambapo msanii Diamond kutoka bongo anayetamba na kibao chake cha Mbagala atakuwepo hapa ukerewere kuanzia mwezi wa November mwaka huu. Wasanii wengine ni Pamoja na First lady wa Urban Pulse Mish Ze Fyah Sis UK Artist anayetamba na single yake Freedom na I don't give a damn.

http://www.youtube.com/watch?v=CVMv053sTiY

Tamasha Hili ni kwa ajili ya kuchangia Vita Dhidi ya Malaria Afrika. Diamond ni ambassador wa Malaria Tanzania na ndiye atakekuwa akiwakilisha.
Shows Hivi zitafanyika tarehe 6th Nov Milton keynes, 12th Nov London and 27th Nov Birmingham.
Stay tune kwa habari zaidi.

Asanteni,

Urban pulse Creative.

MSONDO YARUDI DAR ES SALAAM NA KUANZA MAMBO!



BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Msondo Ngoma , imerejea Dar es Salaam baada ya ziara ya maonyesho matano katika mikoa ya kusini kuanzia Sept 29 mwaka huu ambapo iliweza kukaa huko kwa muda mrefu kwani ni muda mrefu ilikuwa haijaenda kanda hiyo.

Akizungumza Dar es Salaam leo, Msemaji wa bendi hiyo, Rajabu Mhamila 'Super D' amesema ziara hiyo ilikuwa maalumu kwa ajili ya kuitambulisha albamu yao mpya inayoitwa Huna Shukrani.

"Tukiwa huko tulifanya kazi ya kuwapa burudan wapenzi wetu na walipata nafasi ya kuona mambo mengi yanayohusu bendi yao " . Alisema SUPER D.

Ziara hiyo ilianzia ukumbi wa Bwalo la Maendeleo, Kilwa na Hoteli ya Lindi Oktoba Mosi ambapo Oktoba 2 wakatua Brantare Hall na oktoba 3 wakafanya kweli katika ukumbi wa Madeko Masasi, Oktoba 4 Nachingwea na 5 wafanya mambo yao Nyongoro Hall, Ruangwa.

SUPER D aliendelea kufafanua kwamba mbali na utambulisho wa albamu hiyo bendi hiyo pia ilitoa fursa kwa wapenzi wake wa mikao hiyo kusikia vibao vipya vya Dawa ya Deni kulipa na Lipi Jema vilivyoibwa na wasanii mahiri akiwamo Edo Sanga.

Sasa wamerudi kwa kasi zaidi na hali zaidi ya kuisuka bendi hiyo jana usiku walitumbuiza katika viwanja vya TTC Chan'gombe ambapo kwa kiingilio cha 2000 na leo itafanya kweli ukumbi wa Max Bar, Ilala kwa kiingilio cha 500.



BURUDANI MWANZO MWISHO

P.O Box 15493DAR ES SALAAMPhone no. 0713/0754/0787/0774/ 406938

Friday, October 1, 2010

NYOMI LA SLAA

CHADEMA WAKUTANA NA VIONGOZI WA DINI DAR




Mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa (katikati) akisalimiana na Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj Mussa Salum wakati mgombea huyo alipokutana na viongozi mbalimbali wa dini Dar es Salaam jana. Kushoto ni mgombea mwenza, Said Mzee Said. Picha na habari(Mdau).


A
ASKOFU Tomas Laizer wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Kati (kulia), akizungumza na mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA, Dk. Willibroad Slaa, makao makuu ya chama hicho, Kinondoni Dar es Salaam, baada ya ujumbe wa Kamati ya viongozi wa dini nchini akiwemo askofu Laizer, kufanya mazungumzo na viongozi wa CHADEMA jana, ambapo pamoja na mambo mengine walizungumzia mustakabali utakaowezesha uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, kufanyika kwa amani na kutozusha rabsha baada ya matokeo, kwa kuzingatia mambo kadhaa ikiwemo vyama shiriki kukubali matokeo baada ya uchaguzi. Kushoto ni Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, na wa tatu ni mgombea ubunge jimbo la Ubungo kwa tiketi ya Chama hicho, John Myika.